Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Alipofunua Sifa Zake
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • Akiwa kwenye Mlima Sinai, Musa alimsihi Yehova hivi: “Nionyeshe, tafadhali, utukufu wako.” (Kutoka 33:18) Siku iliyofuata, nabii huyo alipata pendeleo la kuuona utukufu wa Mungu.a Musa hakueleza kwa undani mambo aliyoona kwenye maono hayo yenye kuvutia. Badala yake, aliandika maneno ambayo Mungu alisema, ambayo ni muhimu sana. Hebu tuchunguze mambo ambayo Yehova alisema yanayotajwa katika Kutoka 34:6, 7.

      Jambo la kwanza ambalo Mungu anafunua kujihusu ni kwamba yeye ni “Mungu mwenye rehema na neema.” (Mstari wa 6) Kulingana na msomi mmoja, neno la Kiebrania linalotafsiriwa “rehema” linaonyesha “huruma nyororo [za Mungu], kama huruma za baba kwa watoto wake.” Neno linalotafsiriwa “neema” linahusiana na kitenzi “kinachomhusu mtu anayesukumwa na moyo kumsaidia mtu mwenye uhitaji.” Ni wazi kwamba Yehova anataka tujue kuwa anawatunza waabudu wake kama vile wazazi wanavyowatunza watoto wao—kwa kuwaonyesha upendo mwororo na kuhangaikia sana mahitaji yao.—Zaburi 103:8, 13.

      Halafu, Yehova anasema kwamba yeye “si mwepesi wa hasira.” (Mstari wa 6) Hawakasirikii upesi watumishi wake duniani. Badala yake yeye anawaonyesha subira na kuvumilia makosa yao huku akiwapa nafasi ya kubadili mwenendo wao wenye dhambi.—2 Petro 3:9.

      Mungu anaendelea kuzungumza na Musa, akisema kwamba yeye “ni mwingi wa fadhili zenye upendo na kweli.” (Mstari wa 6) Fadhili zenye upendo, au upendo mshikamanifu, ni sifa nzuri ambayo Yehova anatumia kujenga uhusiano thabiti kati yake na watu wake. (Kumbukumbu la Torati 7:9) Yehova pia ni chanzo cha ukweli. Hawezi kudanganya wala kudanganywa. Kwa kuwa yeye ni “Mungu wa ukweli,” tunaamini kabisa yote anayosema, kutia ndani ahadi zake kuhusu wakati ujao.—Zaburi 31:5.

  • Yehova Alipofunua Sifa Zake
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • a Musa hakumwona Yehova moja kwa moja, kwa kuwa hakuna mwanadamu anayeweza kumwona Mungu na kuishi. (Kutoka 33:20) Yaelekea Yehova alimwonyesha Musa maono kuhusu utukufu Wake na alizungumza naye kupitia malaika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki