Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Mfano Bora Sana wa Wema
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
    • 12 Siku iliyofuata wema wa Yehova ulipita mbele ya uso wa Musa kwenye Mlima Sinai. Wakati huo Musa aliona kidogo tu utukufu wa Mungu na kusikia tangazo hili: “BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma [“rehema,” NW], mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema [“fadhili-upendo,” NW] na kweli; mwenye kuwaonea huruma [“ fadhili-upendo,” NW] watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.” (Kutoka 34:6, 7) Maneno hayo yanaonyesha kwamba wema wa Yehova unahusiana na fadhili-upendo zake na sifa nyingine za utu wake. Kuchunguza maneno hayo kutatusaidia kuonyesha sifa ya wema. Na tuchunguze kwanza sifa inayotajwa mara mbili katika tangazo hili zuri kuhusu wema wa Mungu.

  • Yehova Ni Mfano Bora Sana wa Wema
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
    • 13. Katika tangazo kuhusu wema wa Mungu, ni sifa gani ambayo imetajwa mara mbili, na kwa nini jambo hilo linafaa?

      13 ‘BWANA ni Mungu mwingi wa fadhili-upendo; mwenye kuwaonyesha fadhili-upendo watu elfu elfu.’ Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “fadhili-upendo” linamaanisha pia “upendo mwaminifu-mshikamanifu.” Hiyo ndiyo sifa pekee ambayo imetajwa mara mbili katika tangazo la Mungu kwa Musa. Jambo hilo linafaa kama nini kwa kuwa upendo ndiyo sifa kuu ya Yehova! (1 Yohana 4:8) Maneno yanayojulikana sana ya kumsifu Yehova “kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili [“fadhili-upendo,” NW] zake ni za milele,” hukazia sifa hiyo.

  • Yehova Ni Mfano Bora Sana wa Wema
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
    • 19. Ni wonyesho gani wa pekee wa wema ambao Yehova ameonyesha watenda-dhambi wenye kutubu?

      19 ‘BWANA mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi.’ Kwa sababu ya wema wake, Yehova yu tayari kuwasamehe watenda-dhambi wanaotubu. Bila shaka, tunashukuru sana kwamba Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo amefanya iwezekane tusamehewe dhambi kupitia dhabihu ya Yesu. (1 Yohana 2:1, 2) Tu wenye furaha kwelikweli kwamba wote walio na imani katika fidia hiyo wanaweza kufurahia uhusiano wa pekee pamoja na Yehova, wakiwa na tumaini la kuishi milele katika ulimwengu mpya alioahidi. Hizi kwa kweli ni sababu za pekee za kumsifu Yehova kwa kuwaonyesha wanadamu wema wake!—2 Petro 3:13.

      20. Tuna uthibitisho gani kwamba Mungu havumilii ubaya?

      20 “Si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.” Hii kwa kweli ni sababu nyingine ya kumsifu Yehova kwa wema wake. Kwa nini? Kwa sababu jambo moja muhimu kuhusu sifa ya wema ni kwamba hauvumilii ubaya kamwe. Isitoshe, “kwenye ufunuo wa Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika zake wenye nguvu,” kisasi kitalipizwa juu ya “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema.” Hao “watapatwa na adhabu ya kihukumu ya uharibifu udumuo milele.” (2 Wathesalonike 1:6-9) Kisha waabudu wa Yehova watakaookoka wataweza kufurahia maisha kikamili bila kusumbuliwa na watu wasiomwogopa Mungu, “wasio na upendo wa mema.”—2 Timotheo 3:1-3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki