Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Endelea Kuonyesha Sifa ya Wema
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
    • 10. Ni sehemu zipi za wema wa Yehova ambazo zinatajwa kwenye kitabu cha Kutoka 34:6, 7?

      10 Tunaweza ‘kufuliza kufanya lililo jema’ kwa kutumia nuru ya kiroho kutoka katika Neno la Mungu na kwa msaada wa roho takatifu ya Mungu. (Waroma 13:3) Kupitia funzo la Biblia la ukawaida, tunajifunza mengi zaidi kuhusu jinsi tunavyoweza kuiga wema wa Yehova. Makala iliyotangulia ilizungumzia sehemu mbalimbali za wema wa Mungu kama unavyotajwa katika tangazo ambalo Musa aliandika kwenye kitabu cha Kutoka 34:6, 7, ambapo tunasoma: “BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma [“rehema,” NW], mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema [“fadhili-upendo,” NW] na kweli; mwenye kuwaonea huruma [“huwaonyesha fadhili-upendo,” NW] watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.” Tutasaidiwa ‘kufuliza kufanya lililo jema’ kwa kuchunguza sehemu hizi mbalimbali za wema wa Yehova.

  • Endelea Kuonyesha Sifa ya Wema
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 15
    • 14. Kwa nini tuwe wenye kusamehe?

      14 Tangazo la Mungu kwa Musa linapaswa kutuchochea tuwe wenye kusamehe kwa kuwa Yehova yu tayari kusamehe. (Mathayo 6:14, 15) Bila shaka, Yehova huwaadhibu watenda-dhambi wasiotubu. Kwa hiyo, ni lazima tufuate viwango vyake vya wema kuhusiana na kudumisha usafi wa kiroho wa kutaniko—Mambo ya Walawi 5:1; 1 Wakorintho 5:11, 12; 1 Timotheo 5:22.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki