-
Maana ya Kumpenda Jirani YetuMnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 1
-
-
Jirani Yangu Ni Nani?
4. Kulingana na Mambo ya Walawi sura ya 19, Wayahudi walipaswa kuwapenda nani?
4 Alipomwambia Farisayo kwamba amri ya pili iliyo kuu ni kumpenda jirani kama unavyojipenda mwenyewe, Yesu alikuwa akizungumzia sheria hususa ambayo Waisraeli walipewa. Inapatikana katika Mambo ya Walawi 19:18. Katika sura hiyohiyo, Wayahudi waliambiwa kwamba walipaswa kuwaona wengine zaidi ya Waisraeli wenzao kuwa majirani wao. Mstari wa 34 unasema: “Mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni pamoja nanyi atakuwa kwenu kama mwenyeji wenu; nawe utampenda kama wewe mwenyewe, kwa maana mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.” Kwa hiyo, hata watu wasio Wayahudi, hasa wale waliogeuzwa imani, walipaswa kutendewa kwa upendo.
-
-
Maana ya Kumpenda Jirani YetuMnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 1
-
-
Maana ya Kumpenda Jirani Yetu
8. Kulingana na Mambo ya Walawi sura ya 19, upendo ulipaswa kuonyeshwa jinsi gani?
8 Kumpenda jirani, kama vile kumpenda Mungu, si hisia tu; ni jambo linaloonyeshwa kwa matendo. Inafaa kuchunguza mistari mingine inayozunguka amri iliyoandikwa katika Mambo ya Walawi sura ya 19 ambayo inawahimiza watu wa Mungu wampende jirani yao kama wanavyojipenda wenyewe. Tunasoma kwamba Waisraeli waliamriwa wawaruhusu watu wenye kuteseka na wakaaji wageni washiriki katika mavuno. Hawakupaswa kuwaibia, kuwadanganya, au kuwatendea isivyo haki. Waisraeli hawakupaswa kuonyesha ubaguzi katika mambo ya kihukumu. Ingawa walipaswa kukaripia wakosaji ilipohitajiwa, waliagizwa hivi waziwazi: “Usimchukie ndugu yako moyoni mwako.” Amri hiyo na nyingine nyingi zilijumlishwa kwa maneno haya: “Mpende mwenzako kama wewe mwenyewe.”—Mambo ya Walawi 19:9-11, 15, 17, 18.
9. Kwa nini Yehova aliwaamuru Waisraeli wajitenge na mataifa mengine?
9 Ingawa Waisraeli walipaswa kuwapenda wengine, walipaswa pia kujitenga na watu ambao waliabudu miungu ya uwongo. Yehova aliwaonya kuhusu hatari na matokeo ya kuwa na mashirika mabaya. Kwa mfano, Yehova aliamuru hivi kuhusu mataifa ambayo Waisraeli wangemiliki nchi zao: “Usifanye mapatano yoyote ya ndoa pamoja nao. Binti yako usimpe mwana wake, wala binti yake usimchukue kwa ajili ya mwana wako. Kwa maana atamgeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine; na hasira ya Yehova itawaka kwelikweli juu yenu.”—Kumbukumbu la Torati 7:3, 4.
-