-
Yubile ya Yehova—Wakati Wetu Kufurahi SanaMnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
-
-
3. Yubile ilikuwa nini, na ni jambo gani lililotukia wakati huo?
3 Kifungu kilichotajwa juu kinatumia neno “Yubile.” Yubile kilikuwa kipindi cha kushika Sabato cha mwaka mmoja kwa nchi ya Israeli. Kilifuata mfululizo wa miaka saba-saba ya Sabato za ukulima ambayo ilijumlika kuwa muda wa miaka 49. Mwaka wa 50, ile Yubile, ulikuwa ndio upeo wa mfululizo wa miadhimisho ya Sabato kwa nchi ambayo Yehova alikuwa amewapa watu wake, ikitimiza ahadi aliyopewa Abrahamu baba yao ya zamani, “rafiki ya Yehova.” (Yakobo 2:23; Isaya 41:8, NW) Katika siku ya Yubile, uhuru ulitangazwa katika sehemu zote za nchi. Jambo hilo lilimaanisha uhuru kwa Waisraeli wote waliokuwa wamejiuza katika utumwa kwa sababu ya deni. Jambo jingine la Yubile lilikuwa kwamba mali zote za urithi wa mashamba zilizokuwa zimeuzwa (inaelekea kwa sababu ya uchumi wa watu kuharibika) zilirudishwa kwao.—Walawi 25:1-54.
4. Yubile ilitangazwa wakati gani, na jinsi gani?
4 Tukiwa na habari hizo za msingi, unaweza kuthamini ni kwa sababu gani Yubile ulikuwa mwaka wa uhuru wenye kusherehekewa. Ulitangazwa kwa kupiga mbiu katika Siku ya Upatanisho.a Ni kama vile Musa alivyoandika katika Walawi 25:9, 10, NW: “Na wewe ni lazima uililishe mbiu ya mlio mkubwa katika mwezi wa saba katika siku ya kumi ya mwezi; katika siku ya upatanisho ninyi watu mnapaswa kuililisha. Na nyini ni lazima mtakase mwaka wa hamsini na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakaaji wayo wote. Utakuwa Yubile kwa ajili ya ninyi, na lazima mrudi kila mmoja kwenye mali yake na kila mmoja kwa jamaa yake.” Katika 1473 K.W.K, Yoshua aliongoza Waisraeli akawavusha Mto Yordani na kuwaingiza katika Nchi ya Ahadi, ambamo walipaswa kuishika Yubile.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
-
-
Kwanza, Torati ya Musa ilitaka kwamba kila mwaka wa saba uwe sabato kwa ajili ya nchi; mazao hayakupasa kupandwa, kupaliliwa, wala kuvunwa. Baada ya Sabato ya saba ya kila miaka saba-saba (mwaka wa 49), ulikuja mwaka wa pekee wa Yubile, ule mwaka wa 50. Hiyo ilikuwa sabato ambayo katika hiyo nchi ilipasa tena kupumzika. Lililo la maana zaidi, uhuru ulitangazwa. Waebrania waliokuwa wamejiuza ndani ya utumwa waliwekwa huru wasiwe na wajibu wa kulipa madeni na wa kutoa utumishi. Pia, jamaa zilizokuwa zimelazimishwa kuuza mashamba ya urithi zilirudishiwa. Kwa hiyo, kwa Waisraeli Yubile ulikuwa wakati wa kufunguliwa na kurudishwa kwenye hali za kwanza.—Walawi 25:1-46.
Pili, uchunguzi wa kuhusu utimizo wa unabii wa Biblia na kuhusu mahali tulipo sisi katika mtiririko wa wakati unaonyesha kwa uthabiti kwamba ‘siku za uumbaji’ (Mwanzo, sura ya 1) zina urefu wa miaka 7,000 mmoja. Inaeleweka kwamba utawala wa Kristo wa miaka elfu utaleta kwenye kikomo ‘siku ya pumziko’ la Mungu la miaka 7,000, ambayo ndiyo ‘siku’ ya mwisho wa juma la uumbaji. (Ufunuo 20:6; Mwanzo 2:2, 3) Kwa kutegemea njia hiyo ya kufikiri, juma la uumbaji lote lingekuwa na urefu wa miaka 49,000.
Kwa kuona ufanani katika tarakimu, watu wengine wamelinganisha ile miaka 49 ya kipindi cha Yubile ya kale na miaka hiyo 49,000 ya ‘juma la uumbaji.’ Kwa kufikiri kwa njia hiyo, wao wamewaza kwamba mwaka wa Yubile wa Israeli (mwaka wa 50) unapaswa uwe ulitangulia kuwa kionyesho au kivuli cha mambo yatakayokuja baada ya mwisho wa lile ‘juma la uumbaji.’
Ijapokuwa hivyo, zingatia kwamba Yubile ulikuwa hasa mwaka wa watu kufunguliwa na kurudishwa katika hali za kwanza. Kwa sehemu kubwa lile juma la uumbaji linahusiana na Dunia-sayari na usitawi wayo. Lakini kwa habari ya kuendelea kutimia kwa kusudi la Mungu kwa wanadamu duniani, tufe (dunia) lenyewe halikuuzwa ndani ya utumwa na hivyo halimo katika uhitaji wa ukombozi. Jamii ya wanadamu ndiyo inayouhitaji, na wanadamu wamekuwapo, si kwa miaka 49,000 bali kwa karibu miaka 6,000. Biblia inaonyesha kwamba wakati fulani baada ya Adamu na Hawa kuumbwa, wao walimwasi Mungu, hivyo wakaingia ndani ya uteka wa dhambi, kutokamilika, na kifo. Kulingana na Warumi 8:20, 21, Yehova Mungu anakusudia kukomboa jamii ya wanadamu wanaoamini watoke katika utumwa huo. Matokeo ni kwamba, waabudu wa kweli duniani ‘watawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata waingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu —Ona pia Warumi 6:23.
Ingawa kikundi kidogo kilichochaguliwa kipelekwe mbinguni kimesamehewa dhambi zao tangu Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, na hivyo tayari kinafurahia Yubile, Maandiko yanaonyesha kwamba ukombozi kwa ajili ya jamii ya wanadamu wanaoamini utatukia wakati wa Utawala wa Mileani wa Kristo. Huo utakuwa wakati ambao yeye atatumia kuelekea jamii ya wanadamu zile faida za dhabihu yake ya ukombozi. Kufikia mwisho wa Mileani wanadamu watakuwa wamekwisha kuinuliwa kwenye ukamilifu wa kibinadamu, wakiwa huru kabisa bila dhambi na kifo walichorithi. Akiisha kukomesha hivyo yule adui ya mwisho (kifo kilichopitishwa kutokana na Adamu), Kristo atamrudishia Babaye ule Ufalme mwishoni mwa ‘juma la uumbaji’ la miaka 49.000 — 1 Wakorintho 15:24-26.
Kama matokeo, kwa jamii ya wanadamu wanaoamini walio na mataraja ya kidunia, ukombozi na kurudishwa katika hali za kwanza ambako kulifanyika katika mwaka wa Yubile katika Israeli wa kale kutakuwa na ulinganifu unaofaa wakati wa Sabato ya Mileani inayokuja. Hapa ndipo ukombozi na kurudishwa katika hali za kwanza utakapopatikana. Jambo hilo litakuwa chini ya utawala wa Kristo, “kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.”—Mathayo 12:8.
-