Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unathamini Uhai Kama Vile Mungu Anavyouthamini?
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • 5, 6. Sheria ya Musa ilionyesha jinsi gani kwamba damu ni takatifu na yenye thamani? (Ona pia sanduku katika ukurasa wa 78.)

      5 Kweli hizo mbili za msingi zinapatikana pia katika Sheria ya Musa. Andiko la Mambo ya Walawi 17:10, 11 linasema: “Mtu yeyote . . . atakayekula namna yoyote ya damu, nitauweka uso wangu dhidi ya nafsi hiyo inayokula damu, nami hakika nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake. Kwa maana nafsi ya mwili iko katika damu, nami mwenyewe nimeiweka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu ndiyo hufanya upatanisho kupitia nafsi iliyo ndani yake.”a—Ona sanduku “Jinsi Damu Inavyofanya Upatanisho.”

      JINSI DAMU INAVYOFANYA UPATANISHO

      Katika Neno la Mungu, damu huonwa kuwa sawa na uhai. Hivyo, badala ya kuadhibiwa kwa sababu ya kuvunja amri za Yehova, mtenda-dhambi katika Israeli la kale ambaye alionyesha toba angeweza kutoa dhabihu ya mnyama kwenye madhabahu ya Mungu. (Mambo ya Walawi 4:27-31) Dhabihu hiyo ilifanya upatanisho kwa ajili ya dhambi zake, kwa muda tu.

      Katika Biblia, neno “upatanisho” lina maana ya “kubadilishana” au “kufunika,” kama vile kifuniko kinachofaa kinavyoweza kufunika vizuri chombo fulani. Bila shaka, hakuna mnyama yeyote ambaye angeweza “kufunika,” au kufanya upatanisho kikamili kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Hata hivyo, dhabihu za wanyama ziliwakilisha dhabihu kamilifu ya upatanisho ambayo ingetolewa baadaye.—Waebrania 10:1, 4.

      Upatanisho huo ulitolewa “kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.” (Waebrania 10:10) Uhai mkamilifu wa Kristo, unaowakilishwa na “damu [yake] yenye thamani, kama ile ya mwana-kondoo asiye na dosari na asiye na doa,” unalingana kabisa na uhai ambao Adamu aliupoteza. (1 Petro 1:19) Hivyo, haki ilitekelezwa katika njia bora na yenye upendo zaidi, nao “ukombozi [wetu] wa milele” ukawezekana.—Waebrania 9:11, 12; Yohana 3:16; Ufunuo 7:14.

  • Je, Unathamini Uhai Kama Vile Mungu Anavyouthamini?
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • a Kuhusu taarifa ya Mungu ya kwamba “nafsi ya mwili iko katika damu,” gazeti moja linasema kwamba ingawa ni kweli damu inatumiwa kwa njia ya mfano kuwakilisha uhai, “taarifa hiyo ni kweli kihalisi: kila aina tofauti ya chembe za damu inahitajika ili kuendeleza uhai.”—Scientific American.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki