-
“Mwimbieni Yehova”!Igeni Imani Yao
-
-
Yehova huwatia nidhamu wale anaowapenda. (Waebrania 12:5, 6) Alimpenda Miriamu sana hivi kwamba asingemruhusu aendelee kuwa na kiburi. Miriamu aliumia aliporekebishwa, lakini kufanya hivyo kulimwokoa. Kwa sababu alikubali nidhamu kwa imani, alipata tena kibali cha Mungu. Aliendelea kuishi hadi karibu na mwisho wa safari ya Waisraeli nyikani. Huenda alikuwa anakaribia umri wa miaka 130 alipokufa huko Kadeshi katika nyika ya Zini.b (Hesabu 20:1) Karne nyingi baadaye, kwa upendo Yehova alimsifu Miriamu kwa utumishi wake mwaminifu. Kupitia nabii wake Mika, aliwakumbusha watu wake hivi: “Kutoka katika nyumba ya utumwa niliwakomboa; nilimtuma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.”—Mika 6:4.
Imani ya Miriamu ilimwezesha kuendelea kuwa mnyenyekevu Yehova alipomtia nidhamu
-
-
“Mwimbieni Yehova”!Igeni Imani Yao
-
-
b Wote watatu walikufa kwa mfuatano waliozaliwa—kwanza Miriamu, kisha Haruni, halafu Musa—inaonekana ndani ya mwaka uleule.
-