Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Macho Yako Yanamtazama Nani?
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Julai
    • 9. Musa alipokea maagizo gani, lakini alitendaje? (Tazama picha mwanzoni mwa makala hii.)

      9 Musa alitendaje uasi huo ulipotokea? Kwa mara nyingine tena alimtazama Yehova ili ampe mwongozo. Lakini wakati huu Yehova hakumwambia aupige mwamba. Alimwambia Musa achukue fimbo, awakusanye watu mbele ya mwamba, na kisha azungumze na mwamba. (Hes. 20:6-8) Hata hivyo, Musa hakuzungumza na mwamba huo. Badala yake, aliwaka hasira na kuwakemea watu waliokuwa wamekusanyika kwa kusema hivi: “Sikilizeni sasa, enyi waasi! Je, ni lazima tuwatolee maji katika mwamba huu?” Kisha akaupiga mwamba huo si mara moja tu, bali akaupiga mara mbili.—Hes. 20:10, 11.

  • Macho Yako Yanamtazama Nani?
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Julai
    • JINSI MUSA ALIVYOASI

      12. Huenda ni sababu gani nyingine iliyomfanya Yehova awakasirikie vikali Musa na Haruni?

      12 Kuna sababu nyingine ambayo huenda ilimfanya Yehova awakasirikie vikali Musa na Haruni. Ona jinsi Musa alivyowaambia watu: “Je, ni lazima tuwatolee maji katika mwamba huu?” Aliposema “tuwatolee,” huenda Musa alikuwa akimaanisha yeye na Haruni. Maneno hayo yalionyesha ukosefu mkubwa wa heshima kwa Yehova akiwa Chanzo halisi cha muujiza huo. Ukweli wa kwamba huenda Musa hakuonyesha heshima unathibitishwa na maneno ya Zaburi 106:32, 33: “Walimkasirisha kwenye maji ya Meriba, na mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao. Waliitia uchungu roho yake, naye akaongea bila kufikiri kwa midomo yake.”c (Hes. 27:14) Vyovyote vile, kupitia matendo yake, Musa hakumwelekezea Yehova heshima aliyostahili. Yehova aliwaambia hivi Musa na Haruni: “Ninyi wawili mliasi agizo nililowapa.” (Hes. 20:24) Hiyo ilikuwa dhambi kubwa sana!

      13. Kwa nini hukumu ambayo Yehova alitoa dhidi ya Musa ilikuwa ya haki na isiyo na upendeleo?

      13 Wakiwa viongozi wa watu wa Yehova, Musa na Haruni waliwajibika zaidi mbele za Yehova. (Luka 12:48) Hapo awali, Yehova alikataa kizazi kizima cha Waisraeli kiingie katika nchi ya Kanaani kwa sababu ya uasi wao. (Hes. 14:26-30, 34) Hivyo, Yehova alitenda kwa haki na bila upendeleo kwa kutoa hukumu ileile dhidi ya Musa kwa sababu ya uasi wake. Na kama tu ilivyokuwa kwa Waisraeli wengine walioasi, Musa hakuruhusiwa kuingia katika Nchi ya Ahadi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki