-
“Yehova Anawajua Walio Wake”Mnara wa Mlinzi—2014 | Julai 15
-
-
4. Paulo alikuwa na uhakika gani? Alionyeshaje uhakika huo alipomwandikia Timotheo?
4 Paulo alikuwa na hakika kwamba Yehova anatambua ibada ya kinafiki, na anatambua pia wale Wanaomtii. Paulo alipomwandikia Timotheo chini ya mwongozo wa roho takatifu, alitumia maneno yaliyoonyesha kwamba alikuwa na uhakika kabisa kuhusu jambo hilo. Baada ya kutaja madhara ya kiroho ambayo tayari baadhi ya washiriki wa kutaniko walikuwa wamepata kwa sababu ya waasi-imani, Paulo aliandika hivi: “Hata hivyo, msingi imara wa Mungu unakaa ukiwa umesimama, ukiwa na muhuri huu: ‘Yehova anawajua walio wake,’ na: ‘Kila mtu anayelitaja jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu.’”—2 Tim. 2:18, 19.
-
-
“Yehova Anawajua Walio Wake”Mnara wa Mlinzi—2014 | Julai 15
-
-
6 Paulo alitaja “msingi imara wa Mungu” katika muktadha ambamo alinukuu maneno ya Musa katika Hesabu 16:5 kuhusu Kora na wale waliomuunga mkono. Bila shaka, Paulo alikuwa akirejelea matukio katika siku za Musa ili kumtia moyo Timotheo na kumkumbusha kuhusu uwezo wa Yehova wa kutambua na kukomesha matendo ya uasi. Kora hangeweza kuzuia kusudi la Yehova karne nyingi zilizopita, vivyo hivyo, waasi-imani waliokuwa katika kutaniko hawangeweza kulizuia lisitimie. Paulo hakufafanua kwa undani maana ya “msingi imara wa Mungu.” Hata hivyo, ni wazi kwamba maneno aliyotumia yalimchochea Timotheo kuamini kwa uhakika njia za Yehova.
-
-
“Yehova Anawajua Walio Wake”Mnara wa Mlinzi—2014 | Julai 15
-
-
8, 9. Tunaweza kujifunza nini kutokana na “muhuri” wa mfano aliotaja Paulo?
8 Katika 2 Timotheo 2:19, Paulo anataja msingi wa mfano wenye ujumbe. Ni kana kwamba ujumbe huo umepigwa kwa muhuri. Katika nyakati za kale, kwa kawaida maneno yalichongwa kwenye msingi wa jengo ili kuonyesha mjenzi au mmiliki wa jengo hilo. Paulo ndiye mwandikaji wa kwanza katika Biblia kutumia mfano huo hususa.a Muhuri ulio kwenye “msingi imara wa Mungu” una matangazo mawili. Kwanza, “Yehova anawajua walio wake,” na pili, “Kila mtu anayelitaja jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu.” Maneno hayo ya Paulo yanatukumbusha tunachosoma katika Hesabu 16:5.—Soma.
-