-
“Uendako Nitaenda”Igeni Imani Yao
-
-
23. Ruthu alianza kufikiria nini, na Sheria ya Musa ilitoa maandalizi gani kwa ajili ya maskini? (Ona pia maelezo ya chini.)
23 Wanawake hao walipoanza maisha mapya huko Bethlehemu, Ruthu alianza kufikiria jinsi ambavyo angetimiza mahitaji yake na pia ya Naomi. Alijifunza kwamba Sheria ambayo Yehova alikuwa amewapa watu wake huko Israeli ilitia ndani mpango wenye upendo kwa ajili ya maskini. Waliruhusiwa kwenda mashambani wakati wa mavuno na kuwafuata wavunaji, huku wakikusanya masalio na vilevile kuvuna nafaka kwenye kingo za mashamba.b—Law. 19:9, 10; Kum. 24:19-21.
24, 25. Ruthu alifanya nini alipoingia katika mashamba ya Boazi, na kazi ya kukusanya masalio ilikuwaje?
24 Ulikuwa wakati wa kuvuna shayiri, inaelekea mwezi wa Aprili kulingana na kalenda ya kisasa, na Ruthu alienda mashambani ili kuona kama kuna mtu ambaye angemruhusu akusanye masalio. Aliingia katika shamba la mwanamume aliyeitwa Boazi, tajiri mwenye mashamba ambaye alikuwa mtu wa ukoo wa Elimeleki, mume wa Naomi aliyekuwa amekufa. Ingawa Sheria ilimruhusu kukusanya masalio, hakutumia maandalizi hayo vibaya, alimwomba ruhusa mwanamume aliyewasimamia wavunaji ili aanze kukusanya. Alimruhusu, na Ruthu akaanza kazi.—Rut. 1:22–2:3, 7.
-
-
“Uendako Nitaenda”Igeni Imani Yao
-
-
b Ilikuwa sheria ya pekee sana, tofauti kabisa na mpango wowote ambao Ruthu alijua katika nchi yao. Zamani, katika Mashariki ya Karibu, wajane walitendewa vibaya. Kitabu kimoja cha marejezo kinasema: “Baada ya kufiwa na mumewe, kwa kawaida mjane angetegemea wanawe; kama hakuwa na wana, huenda angejiuza awe mtumwa, angefanya ukahaba, au kufa.”
-