-
“Uendako Nitaenda”Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
Wanawake hao walipoendelea na maisha huko Bethlehemu, Ruthu alianza kufikiria jinsi ambavyo angetimiza mahitaji yake na ya Naomi pia. Alijifunza kwamba Sheria ambayo Yehova alikuwa amewapa watu wake huko Israeli ilitia ndani mpango wenye upendo kwa ajili ya maskini. Waliruhusiwa kwenda mashambani wakati wa mavuno na kuwafuata wavunaji, huku wakikusanya masalio yaliyobaki na vilevile kuvuna nafaka iliyokua kwenye ukingo wa mashamba.c—Mambo ya Walawi 19:9, 10; Kumbukumbu la Torati 24:19-21.
Ulikuwa wakati wa kuvuna shayiri, inaelekea ulikuwa mwezi wa Aprili kulingana na kalenda ya kisasa, na Ruthu alienda mashambani ili kuona kama kuna mtu ambaye angemruhusu akusanye masalio nyuma ya wavunaji. Aliingia katika shamba la mwanamume aliyeitwa Boazi, tajiri aliyekuwa na mashamba na ambaye alikuwa mtu wa ukoo wa Elimeleki, mume wa Naomi aliyekuwa amekufa. Ingawa Sheria ilimruhusu kukusanya masalio, hakuona kwamba ilikuwa haki yake, alimwomba ruhusa mwanamume aliyewasimamia wavunaji ili aanze kazi ya kukusanya. Alimruhusu, na Ruthu akaanza kazi.—Ruthu 1:22–2:3, 7.
-
-
“Uendako Nitaenda”Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
c Ilikuwa sheria ya pekee sana, bila shaka, ilikuwa tofauti na mpango wowote ambao Ruthu alijua katika nchi yao. Zamani, katika Mashariki ya Karibu, wajane walitendewa vibaya. Kitabu kimoja cha marejezo kinasema hivi: “Baada ya kufiwa na mumewe, kwa kawaida mjane angetegemea wanawe ili kupata mahitaji; kama hakuwa na wana, huenda angejiuza awe mtumwa, angefanya ukahaba, au afe.”
-