-
Alimweleza Mungu Mahangaiko YakeIgeni Imani Yao
-
-
15, 16. (a) Hana alihisije baada ya kumwabudu na kumweleza Yehova mahangaiko yake kwenye maskani? (b) Tunawezaje kuiga mfano wa Hana tunapokabiliana na hisia zisizofaa?
15 Hana alipomweleza Yehova mahangaiko yake na kumwabudu katika maskani, alihisije? Simulizi hilo linasema: “Mwanamke huyo akaenda zake, akala chakula, na uso wake haukuonyesha tena kuhangaika.” (1 Sam. 1:18) Biblia Habari Njema inasema: “Hakuwa na huzuni tena.” Hana alihisi utulivu. Ni kana kwamba alikuwa amechukua mzigo wake wa kihisia na kumtupia Yehova, Baba yake wa mbinguni mwenye nguvu. (Soma Zaburi 55:22.) Je, Yehova anaweza kushindwa na tatizo lolote? La—hajawahi kushindwa na kamwe hatashindwa!
16 Tunapohisi tumelemewa na hisia au kuhuzunika kupita kiasi, tunaweza kumwiga Hana na kuzungumza waziwazi na Mungu ambaye Biblia inamwita “Msikiaji wa sala.” (Zab. 65:2) Tukisali kwa imani, huenda tukaacha kuhuzunika na badala yake tukawa na “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Flp. 4:6, 7.
-
-
Alimweleza Mungu Mahangaiko YakeIgeni Imani Yao
-
-
18 Ni wakati gani ambapo Penina alitambua hangeweza tena kumhuzunisha Hana? Simulizi hilo halitaji, lakini maneno uso wa Hana “haukuonyesha tena kuhangaika” yanaonyesha kuanzia wakati huo Hana alikuwa mwenye furaha. Vyovyote vile, baada ya muda mfupi Penina aligundua hangeweza tena kumhuzunisha Hana. Baada ya hapo, Biblia haimtaji Penina tena.
-