Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mjane wa Sarefathi Alithawabishwa kwa Sababu ya Imani Yake
    Mnara wa Mlinzi—2014 | Februari 15
    • Yehova alikusudia kuleta ukame wa muda mrefu katika ufalme wa Ahabu, mfalme mwovu wa Israeli. Baada ya Eliya kutangaza kwamba kungekuwa na ukame, Mungu alimficha ili Ahabu asimwangamize na pia alimlisha kimuujiza nabii huyo kwa kumpa mkate na nyama zilizoletwa na kunguru. Kisha, Yehova alimwambia Eliya hivi: “Ondoka, nenda Sarefathi, wa Sidoni, nawe ukae huko. Tazama! Nitamwamuru mwanamke fulani huko, mjane, akupe chakula.” —1 Fal. 17:1-9.

  • Mjane wa Sarefathi Alithawabishwa kwa Sababu ya Imani Yake
    Mnara wa Mlinzi—2014 | Februari 15
    • Mjane huyo alijua kwamba Eliya ni Mwisraeli aliyemwogopa Mungu. Maneno haya aliyosema yanaonyesha hivyo: “Kama anavyoishi Yehova Mungu wako.” Inaonekana kwamba alimjua Yehova, Mungu wa Israeli kwa kadiri fulani ingawa hakumwita ‘Mungu wake.’ Aliishi Sarefathi, mji “wa” Sidoni au uliotegemea jiji la Sidoni huko Foinike. Inaelekea kwamba wakaaji wa Sarefathi waliabudu Baali. Hata hivyo, Yehova aliona sifa fulani ya pekee ya mjane huyo.

      Mjane maskini wa Sarefathi alionyesha imani licha ya kwamba aliishi miongoni mwa watu walioabudu sanamu. Yehova alimtuma Eliya kwa mjane huyo ili wote wawili waokolewe. Tunajifunza jambo muhimu kutokana na hilo.

      Baadhi ya wakaaji wa Sarefathi walioabudu Baali hawakuwa na moyo mwovu. Yehova alipomtuma Eliya kwa mjane huyo, alionyesha kwamba Anaona watu wenye nia njema ambao hawajaanza Kumtumikia. Kwa kweli, “katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa [Mungu] na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”—Mdo. 10:35.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki