-
Ashuru Yenye Ukatili Ile Serikali Kubwa ya Pili ya UlimwenguMnara wa Mlinzi—1988 | Februari 15
-
-
Biblia inasema kwamba “Senakeribu mfalme wa Ashuru alikuja akapanda dhidi ya miji yote ya Yuda yenye ngome na kuibamba.” Kwa kuogopeshwa sana na tisho hilo, Mfalme Hezekia wa Yerusalemu ‘alituma ujumbe kwa mfalme wa Ashuru kule Lakishi’ na akajitolea kununua mwondoko wa mfalme huyo kwa kumpa zawadi nyingi sana za heshima.—2 Wafalme 18:13, 14, NW.
-
-
Ashuru Yenye Ukatili Ile Serikali Kubwa ya Pili ya UlimwenguMnara wa Mlinzi—1988 | Februari 15
-
-
Bila shaka, Senakeribu mwenye moyo uliotukuka hangetazamiwa kujisifu juu ya hasara hiyo ya vikosi vyake. Lakini jambo ambalo yeye anasema ni la kupendeza. Habari zake za matukio ya kila mwaka, ambazo zimeandikwa katika ile Prizimu ya Taasisi ya Nchi za Mashariki na pia ile Prizimu ya Taylor, zinasema: “Kwa habari ya Hezekia Myahudi, yeye hakujiweka chini ya nira yangu, Mimi nililaza mazingiwa kwa 46 ya miji yake imara, ngome za ukuta na kwa vijiji vidogo visivyohesabika katika ujirani wao, na kushinda (hivyo) . . . Yeye mwenyewe mimi nilifanya mfungwa-gereza katika Yerusalemu, kao lake la kifalme, kama ndege katika kizimba chake.” Senakeribu anasema kwamba “ile fahari yenye kutia hofu nyingi ya ubwana wangu” ililemea Hezekia. Hata hivyo, yeye hasemi aliteka Hezekia au alishinda Yerusalemu, kama alivyokuwa amesema juu ya ile ‘miji imara’ na “vijiji vidogo.” Kwa sababu gani sivyo? Kama vile Biblia inavyoonyesha, ile sehemu bora kabisa ya vikosi ambavyo Senakeribu alikuwa amepeleka vikafanye hivyo ilikuwa imeangamizwa!
-