-
Alivumilia Hadi MwishoIgeni Imani Yao
-
-
Kwa unyenyekevu, Eliya alimwachia Yehova ajibu ombi hilo. Ikiwa Yehova angemruhusu Elisha amwone Eliya anapochukuliwa na Mungu, basi Mungu angekuwa amekubali ombi la Elisha. Na punde si punde, marafiki hao wa muda mrefu walipokuwa wakitembea “huku wakizungumza,” jambo lenye kustaajabisha likatokea!—2 Wafalme 2:10,11.
Urafiki wa Eliya na Elisha uliwasaidia wote wawili kuvumilia hali ngumu
Mwangaza wa ajabu ulionekana angani na ukakaribia zaidi na zaidi. Tunaweza kuwazia mngurumo na sauti ya dhoruba ya upepo iliyotokea ghafla, ikifuatiwa na kitu kinachong’aa kilichowakaribia wanaume hao wawili na kuwalazimisha kutengana, labda kwa sababu walichoona kiliwafanya warudi nyuma kwa mshangao. Waliona gari la kukokotwa, liking’aa kana kwamba limefanyizwa kwa moto. Eliya alijua kwamba wakati wake ulikuwa umefika. Je, alipanda gari hilo? Simulizi hilo halisemi. Vyovyote vile, alijihisi akipandishwa juu, juu zaidi angani, na kubebwa na dhoruba hiyo!
-
-
Alivumilia Hadi MwishoIgeni Imani Yao
-
-
Eliya alienda wapi baada ya hapo? Dini fulani zinafundisha kwamba alichukuliwa mbinguni akaishi na Mungu. Lakini hilo haliwezekani. Karne kadhaa baadaye, Yesu Kristo alisema kwamba hakuna mtu yeyote aliyekuwa amepanda kwenda mbinguni kufikia wakati huo. (Yohana 3:13) Kwa hiyo, tunaposoma kwamba “Eliya akapanda kuelekea mbinguni katika dhoruba ya upepo,” lazima tujiulize, Ni mbingu zipi hizo? (2 Wafalme 2:11) Mbali tu na kuwakilisha makao ya Yehova, Biblia inatumia neno “mbingu” kuwakilisha maeneo ya angani yanayozunguka dunia yetu, ambako mawingu hufanyizwa na ndege huruka. (Zaburi 147:8) Eliya alipanda kuelekea mbingu hizo, yaani, alipanda angani. Kisha akaenda wapi?
Yehova alimhamisha nabii huyo mpendwa hadi kwenye mgawo mpya, kwenye ufalme jirani wa Yuda. Biblia inaonyesha kwamba Eliya alikuwa bado akifanya kazi huko, miaka saba hivi baadaye. Mfalme Yehoramu mwovu ndiye aliyekuwa akitawala Yuda wakati huo. Alikuwa amemwoa binti ya Ahabu na Yezebeli, kwa hiyo uvutano wao mwovu bado ulikuwepo. Yehova alimwagiza Eliya aandike barua ya kutangaza hukumu juu ya Yehoramu. Kama ilivyotabiriwa, Yehoramu alikufa kifo kibaya sana. Na jambo baya hata zaidi ni kwamba simulizi hilo linamalizia kwa kusema: “Hakuna mtu yeyote aliyesikitishwa na kifo chake.”—2 Mambo ya Nyakati 21:12-20.
-