Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msikiaji wa Sala”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 1
    • JE, KWELI Yehova Mungu hujibu sala za unyofu za waabudu waliojitoa kwake? Simulizi la Biblia kuhusu mtu asiyejulikana sana aitwaye Yabesi, linaonyesha kuwa Yehova kwa kweli ni “msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Simulizi hilo fupi linapatikana mahali ambapo mtu hangetazamia kulipata—katika orodha za kiukoo zinazopatikana mwanzoni mwa kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati. Acheni tuchunguze 1 Mambo ya Nyakati 4:9, 10.

      Mambo yote tunayojua kumhusu Yabesi yanapatikana katika mistari hiyo miwili. Kulingana na mstari wa 9, mama yake ‘alimwita jina Yabesi, akisema: “Nimemzaa kwa maumivu.”’a Kwa nini alichagua jina hilo? Je, alimzaa mwana huyo kwa maumivu makali zaidi kuliko ilivyo kawaida? Je, labda alikuwa mjane aliyehuzunika kwamba mumewe hakuwa hai kumwona mtoto wao mchanga? Biblia haijibu maswali hayo. Lakini siku moja mama huyo angekuwa na sababu ya kujivunia mtoto wake. Huenda ndugu za Yabesi walikuwa watu wenye kuheshimika, lakini “Yabesi a[liku]ja kuheshimika kuliko ndugu zake.”

  • “Msikiaji wa Sala”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 1
    • a Jina Yabesi linatokana na neno linaloweza kumaanisha “maumivu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki