-
Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
3. Wayahudi walikuwa wamekosa kujua nini kwa habari ya kusudi la kurudi kwao kutoka uhamishoni?
3 Kwa nini Yehova alimpa Hagai utume? Kwa sababu hii: Katika 537 K.W.K., Koreshi alikuwa ametoa amri iliyoruhusu Wayahudi warudie bara la kwao kujenga upya nyumba ya Yehova. Lakini sasa ilikuwa 520 K.W.K., na hekalu lilikuwa mbali na kukamilishwa. Muda wa miaka yote hiyo Wayahudi walikuwa wameacha vipingamizi vya adui pamoja na ubaridi wao wenyewe na ufuatiaji vitu vya kimwili uwazuie kutimiza kusudi lenyewe la kurudi kwao.—Ezra 1:1-4; 3:10-13; 4:1-24; Hag. 1:4.
4. Ni nini kilichokuwa kimezuia ujenzi wa hekalu, lakini ni mambo gani yaliyotukia wakati Hagai alipoanza kutoa unabii?
4 Kama vile maandishi yanavyoonyesha, mara tu msingi wa hekalu ulipowekwa (katika 536 K.W.K.) “watu wa nchi wakaidhoofisha mikono ya watu wa Yuda, wakawasumbua [wakiwavunja moyo, NW], walipokuwa wakijenga. Wakawaajiri washauri juu yao, ili kuwapinga kusudi lao.” (Ezra 4:4, 5) Hatimaye, katika 522 K.W.K., wapinzani hao wasio Wayahudi walifaulu kufanya kuwepo marufuku rasmi juu ya kazi. Ilikuwa katika mwaka wa pili wa utawala wa mfalme Mwajemi Dario Haistaspo, yaani, katika 520 K.W.K., kwamba Hagai akaanza kutoa unabii, na hiyo iliwatia moyo Wayahudi warudie ujenzi wa hekalu. Ndiposa, Dario akapelekewa barua na maliwali jirani wakiomba kwamba shauri likatwe kuhusu jambo hilo; Dario alihuisha ile amri ya Koreshi na kuwaunga mkono Wayahudi juu ya adui zao.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
8. Kwa nini Wayahudi hawabarikiwi na Yehova kwa vitu vya kimwili?
8 Ujumbe wa kwanza (1:1-15). Huu waelekezwa kwa Liwali Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yoshua, lakini masikioni mwa watu hao. Watu hao wamekuwa wakisema, “Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujengwa nyumba ya BWANA [Yehova, NW].” Kupitia Hagai Yehova auliza swali la kupekua-pekua maoni: “Je! huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?” (1:2, 4) Wao wamepanda mbegu nyingi kwa kufuatia vitu vya kimwili, lakini hawakunufaika sana kwa njia ya chakula, kinywaji, na nguo. “Zitafakarini njia zenu,” Yehova aonya kwa upole. (1:7) Wakati umefika wa kuleta mbao na kujenga nyumba ile, ili Yehova apate kutukuzwa. Wayahudi watunza vizuri nyumba zao wenyewe, lakini nyumba ya Yehova imelala hali ya ukiwa. Kwa hiyo, Yehova amekuwa mnyimivu ili umande wa mbinguni na ongezeko la shambani na baraka yake visiwe juu ya mwanadamu na jasho lake.
9. Yehova achocheaje Wayahudi wafanye kazi?
9 Kumbe, wameelewa! Hagai hakutoa unabii bure. Watawala na watu waanza ‘kutii sauti ya Yehova, Mungu wao.’ Hofu kwa Yehova yawa badala ya hofu kwa mwanadamu. Uhakikishio wa Yehova kupitia Hagai mjumbe wake ni kwamba: “Mimi nipo pamoja nanyi.” (1:12, 13) Yehova mwenyewe ndiye anayeamsha roho ya liwali, roho ya kuhani mkuu, na roho ya baki la watu Wake. Waanza kazi, siku 23 tu baada ya Hagai kuanza kutoa unabii na kujapokuwa na marufuku rasmi ya serikali ya Uajemi.
-