Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zingatia Kazi za Mungu za Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
    • 3. Mungu aliuliza juu ya mambo gani kwenye Ayubu 38:22-23, 25-29?

      3 Wakati mmoja, Mungu alimwuliza Ayubu hivi: “Je! umeziingia ghala za theluji, au umeziona ghala za mvua ya mawe, nilizoziweka akiba kwa wakati wa misiba, kwa siku ya mapigano na vita?” Theluji na mvua ya mawe hutokea katika sehemu nyingi za dunia yetu. Mungu aliendelea kumwuliza: “Ni nani aliyepasua mfereji kwa maji ya gharika, au njia kwa umeme wa radi; kunyesha mvua juu ya nchi isiyo na watu; juu ya jangwa asiyokaa mwanadamu; kuishibisha nchi iliyo kame na ukiwa, na kuyameza majani yaliyo mororo? Je! mvua ina baba au ni nani aliyeyazaa matone ya umande? Barafu ilitoka katika tumbo la nani na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa?”—Ayubu 38:22, 23, 25-29.

  • Zingatia Kazi za Mungu za Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
    • 7. Mwanadamu ana ujuzi mwingi kadiri gani kuhusu mvua?

      7 Namna gani mvua? Mungu alimwuliza Ayubu hivi: “Je! mvua ina baba? Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande?” Ensaiklopidia hiyohiyo yasema hivi: ‘Ni vigumu kwa wanasayansi kueleza jinsi ambavyo mawingu na matone ya mvua hutokea kwa sababu kuna utendaji mwingi tata katika angahewa na kiwango cha mvuke na chembe zilizo hewani hubadilika-badilika.’ Kwa maneno sahili, wanasayansi wametoa dhana zenye maelezo mengi, lakini hawawezi kueleza kikamili jinsi ambavyo mvua hutokea. Hata hivyo, unajua kwamba mvua ambayo ni muhimu hunyesha na kuitia dunia maji. Husitawisha mimea na hutuwezesha kuishi na kufurahia maisha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki