-
Tunawezaje Kuwa Safi Machoni pa Mungu?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Ili tuwe safi, tunapaswa kuepuka mazoea gani?
Biblia inatuhimiza “tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho.” (2 Wakorintho 7:1) Hivyo, tunajitahidi kuepuka jambo lolote linaloweza kuchafua mwili au akili zetu. Mawazo yetu yanapaswa kumfurahisha Yehova, basi tunajitahidi kabisa kuepuka mawazo yasiyofaa. (Zaburi 104:34) Pia, tunajitahidi kuepuka maneno machafu.—Soma Wakolosai 3:8.
Ni nini kingine kinachoweza kutuchafua kimwili au kiadili? Kuna vitu vinavyoweza kuchafua mwili wetu. Kwa hiyo, tunaepuka kuvuta sigara, kutumia tumbaku, kutafuna miraa au mirungi, na kutumia dawa za kulevya. Tunapoepuka vitu hivyo, tunakuwa na afya bora na tunaonyesha kwamba tunaheshimu zawadi ya uhai. Pia, tunajitahidi kuwa na maadili safi kwa kuepuka mazoea machafu kama vile kupiga punyeto na kutazama ponografia. (Zaburi 119:37; Waefeso 5:5) Inaweza kuwa vigumu kushinda mazoea hayo, lakini Yehova anaweza kutusaidia kuyashinda.—Soma Isaya 41:13.
-
-
Tunawezaje Kuwa Safi Machoni pa Mungu?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Jitahidi kushinda mawazo na mazoea machafu
Soma Wakolosai 3:5, kisha mzungumzie maswali haya:
Tunajuaje kwamba kutazama ponografia, kutuma ujumbe au picha za ngono, na kupiga punyeto ni mazoea machafu machoni pa Yehova?
Je, inawezekana kufuata sheria za Yehova kuhusu usafi wa maadili? Kwa nini?
Jifunze jinsi ya kushinda mawazo machafu. Onyesha VIDEO.
Yesu alitoa mfano unaoonyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua thabiti ili tuendelee kudumisha maadili safi. Soma Mathayo 5:29, 30, kisha mzungumzie swali hili:
Ingawa Yesu hakumaanisha tunapaswa kujisababishia majeraha ya kimwili, alionyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua fulani. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani thabiti ili kuepuka mawazo machafu?b
Ikiwa unapambana ili kushinda mawazo machafu, Yehova anathamini jitihada zako. Soma Zaburi 103:13, 14, kisha mzungumzie swali hili:
Ikiwa unapambana na zoea chafu, andiko hili linawezaje kukusaidia uendelee kupambana?
Usife moyo, endelea kupambana!
Huenda ukajiambia hivi, ‘Nimeshindwa, hakuna haja ya kuendelea kupambana.’ Lakini fikiria jambo hili: Mkimbiaji anapoanguka haimaanishi kwamba hawezi kuendelea na mbio hizo, pia haimaanishi kwamba anapaswa kurudi nyuma na kuanza tena. Vivyo hivyo, hata unapolemewa na kurudia zoea hilo, haimaanishi kwamba huwezi kulishinda. Wala haimaanishi kwamba jitihada ulizofanya ni za bure. Ni jambo la kawaida kujikwaa. Lakini usife moyo! Kwa msaada wa Yehova, unaweza kushinda zoea baya.
-