Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Somo la 8. Mwanamume ameketi akitazama angani.

      SOMO LA 08

      Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova

      Yehova anataka umjue vizuri. Kwa nini? Anatarajia kwamba kadiri unavyojifunza kuhusu sifa zake, njia zake na kusudi lake, ndivyo utakavyotamani kuwa rafiki yake. Je, wewe unaweza kuwa rafiki ya Mungu? (Soma Zaburi 25:14.) Unapaswa kufanya nini ili uwe rafiki yake? Biblia inajibu maswali hayo na inaeleza kwa nini urafiki pamoja na Yehova ndio urafiki bora zaidi kuliko urafiki mwingine wowote.

      1. Yehova anakualika ufanye nini?

      ‘Mkaribie Mungu, naye atakukaribia.’ (Yakobo 4:8) Hilo linamaanisha nini? Yehova anakualika uwe rafiki yake. Huenda watu fulani wakafikiri kwamba ni vigumu kuwa rafiki ya Mungu kwa sababu hawawezi kumwona. Hata hivyo, katika Neno lake Biblia, Yehova ameeleza mambo yote tunayohitaji kujua kuhusu sifa zake ili tusitawishe urafiki pamoja naye. Tunaposoma ujumbe wa Mungu katika Biblia, urafiki wetu pamoja naye huzidi kukua, ingawa hatujawahi kumwona.

      2. Kwa nini Yehova ndiye Rafiki bora zaidi kuliko rafiki mwingine yeyote?

      Yehova anakupenda kuliko mtu mwingine yeyote. Anataka uwe na furaha na uzungumze naye wakati wowote unapohitaji msaada. Unaweza ‘kumtupia mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakujali.’ (1 Petro 5:7) Sikuzote Yehova yuko tayari kuwasaidia, kuwafariji, na kuwasikiliza rafiki zake.​—Soma Zaburi 94:18, 19.

      3. Yehova anatarajia rafiki zake wafanye nini?

      Yehova anawapenda watu wote, “lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.” (Methali 3:32) Yehova anatarajia rafiki zake wafanye mambo anayoona kuwa mazuri na waepuke mambo mabaya. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hawawezi kufuata kikamili viwango vya Yehova kuhusu mema na mabaya. Hata hivyo, Yehova anatuelewa vizuri. Anamkubali kila mtu anayempenda kikweli na anayefanya yote anayoweza ili kumfurahisha.​—Zaburi 147:11; Matendo 10:34, 35.

      CHIMBA ZAIDI

      Jifunze mengi kuhusu jinsi unavyoweza kuwa rafiki ya Yehova, na utambue kwa nini yeye ni Rafiki bora zaidi kuliko rafiki mwingine yeyote.

      4. Abrahamu alikuwa rafiki ya Yehova

      Simulizi la Biblia kumhusu Abrahamu (anayeitwa pia Abramu) linatusaidia kuelewa jinsi tunavyoweza kuwa rafiki ya Mungu. Soma kumhusu Abrahamu katika Mwanzo 12:1-4. Kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova alimwambia Abrahamu afanye nini?

      • Yehova alimwahidi nini?

      • Abrahamu alitendaje baada ya kupokea maagizo ya Yehova?

      5. Mambo ambayo Yehova anatarajia kutoka kwa rafiki zake

      Kwa kawaida sisi hutazamia mambo fulani kutoka kwa rafiki zetu.

      • Ni mambo gani ambayo ungependa rafiki zako wakufanyie?

      Soma 1 Yohana 5:3, kisha mzungumzie swali hili:

      • Yehova anatarajia nini kutoka kwa rafiki zake?

      Ili kumtii Yehova, tunapaswa kubadili mwenendo na tabia zetu. Soma Isaya 48:17, 18, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini Yehova anataka rafiki zake wabadili mwenendo na tabia zao?

      Fundi akimpa kofia ya kazi fundi mwenzake.

      Rafiki mzuri hutukumbusha kufanya mambo yanayoweza kutulinda na kutunufaisha. Yehova hufanya vivyo hivyo pia kwa rafiki zake

      6. Jinsi Yehova anavyowasaidia rafiki zake

      Yehova huwasaidia rafiki zake kukabiliana na matatizo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Yehova Amenisaidia Sana (3:21)

      • Yehova amemsaidiaje mwanamke katika video hiyo kukabiliana na mawazo na hisia zisizofaa?

      Soma Isaya 41:10, 13, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova anaahidi kuwafanyia nini rafiki zake wote?

      • Je, unafikiri Yehova ni rafiki mzuri? Kwa nini?

      Picha: Marafiki wa karibu wakisaidiana. 1. Wanaume wakisaidiana kubeba meza. 2. Mwanamke akimweleza mwanamke mwenzake mahangaiko yake. 3. Mwanamume akimsaidia mwenzake aliyevunjika mguu kutembea.

      Rafiki wa karibu watakusaidia unapohitaji msaada. Yehova pia atakusaidia

      7. Ili tuwe rafiki za Yehova tunapaswa kuwasiliana naye

      Mawasiliano huimarisha urafiki. Soma Zaburi 86:6, 11, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Tunaweza kuzungumza na Yehova kupitia njia gani?

      • Yehova huzungumza nasi kupitia njia gani?

      Picha: 1. Mwanamke akisali. Mshale unaoelekea juu. 2. Mwanamke akisoma Biblia. Mshale unaoelekea chini.

      Tunazungumza na Yehova kupitia sala; naye Yehova huzungumza nasi kupitia Biblia

      WATU FULANI HUSEMA: “Haiwezekani kuwa rafiki ya Mungu.”

      • Unaweza kutumia andiko gani kuonyesha kwamba inawezekana kuwa rafiki ya Yehova?

      MUHTASARI

      Yehova anataka kuwa Rafiki yako, na atakusaidia uwe na uhusiano wa karibu pamoja naye.

      Ungejibuje?

      • Yehova huwasaidiaje rafiki zake?

      • Kwa nini Yehova anawaagiza rafiki zake wabadili mwenendo na tabia zao?

      • Je, unafikiri ni vigumu kuwa rafiki ya Yehova? Kwa nini?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Urafiki pamoja na Mungu unaweza kuboreshaje maisha yako?

      “Yehova​—Mungu Tunayepaswa Kumjua” (Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 2003)

      Jifunze jinsi ya kusitawisha urafiki pamoja na Mungu.

      “Ninaweza Kuwa Rafiki ya Mungu Jinsi Gani?” (Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2, sura ya 35)

      Jifunze kwa nini mwanamke huyu anahisi kwamba urafiki wake na Yehova ulibadili maisha yake.

      “Sikutaka Kufa!” (Mnara wa Mlinzi Na. 1 2017)

      Wasikilize vijana wanapoeleza jinsi wanavyohisi kumhusu Yehova.

      Inamaanisha Nini Kuwa Rafiki ya Mungu? (1:46)

  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Tunapobatizwa tunajiunga na familia ya Yehova

      Tunapobatizwa tunajiunga na familia yenye umoja ya ulimwenguni pote. Ingawa tumetoka katika maeneo na malezi mbalimbali, sisi sote tunaamini mambo yaleyale na tunaishi kulingana na viwango vilevile vya maadili. Soma Zaburi 25:14 na 1 Petro 2:17, kisha mzungumzie swali hili:

      • Mtu anapobatizwa anakuwa na uhusiano gani na Yehova na watu wengine wanaomwabudu?

      Picha: Dada aliyebatizwa akifikiria kuhusu uhusiano mzuri alio nao pamoja na wengine kutanikoni. 1. Anamweleza hisia zake dada fulani. 2. Anamsaidia dada aliyezeeka kutembea. 3. Anafurahia chakula pamoja na marafiki wenye umri mbalimbali. 4. Anamhubiria mwanamume akiwa pamoja na dada mwingine. 5. Anapiga picha na Mashahidi wawili kutoka jamii tofauti kwenye kusanyiko.
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 2. Tunawezaje kuwa na maisha yenye kusudi leo?

      Yehova alituumba tukiwa na ‘uhitaji wa kiroho,’ yaani, tamaa ya kumjua na kumwabudu. (Soma Mathayo 5:3-6.) Anataka tuwe na urafiki wa karibu pamoja naye, ‘tutembee katika njia zake zote, tumpende,’ na kumtumikia ‘kwa moyo wetu wote.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12; Zaburi 25:14) Tunapofanya hivyo, tunakuwa na furaha ya kweli hata ingawa tunakabili matatizo. Tunapomwabudu Yehova, maisha yetu yanakuwa na kusudi la kweli kwa sababu tunaishi kulingana na viwango vyake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki