Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Roho
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Kwa kuwa asili ya kani ya uhai, au roho, iliyo ndani ya mwanadamu (vilevile ndani ya uumbaji wa wanyama) haina utu, ni wazi kwamba taarifa ya Daudi kwenye Zaburi 31:5, iliyonukuliwa na Yesu wakati wa kufa kwake (Lu 23:46), “Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako,” ilimaanisha kwamba Mungu alikuwa anaombwa alinde, aitunze, kani ya uhai ya mtu huyo. (Linganisha Mdo 7:59.) Si lazima kuwe na usafirishaji wa kikweli na kihalisi wa kani fulani kutoka kwa sayari hii kwenda mbinguni mbele za uso wa Mungu. Kama vile harufu yenye manukato ya dhabihu za wanyama ilivyosemekana ‘inanuswa’ na Mungu (Mwa 8:20, 21), ilihali harufu hiyo bila shaka ilibaki ndani ya angahewa la dunia, ndivyo, pia Mungu angeweza ‘kukusanya,’ au angeweza kukubali ni kana kwamba amekabidhiwa, roho au kani ya uhai katika maana ya kitamathali, yaani, bila ya kuwa na usafirishaji wa kihalisi wa kani ya uhai kutoka duniani. (Ayu 34:14; Lu 23:46) Basi, ni wazi mtu kukabidhiana roho yake inamaanisha kwamba yeye anaweka tumaini lake katika Mungu amrudishie yeye mwenyewe wakati ujao kani hiyo ya uhai kupitia ufufuo.—Linganisha Hes 16:22; 27:16; Ayu 12:10; Zb 104:29, 30.

  • Kweli
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Roho ya Mungu ingewafundisha kila jambo walilohitaji kujua ili kutimiza kazi yao, kuwakumbusha na kufungua uelewaji wao wa mambo waliyokuwa hapo awali wameyasikia kutoka kwa Yesu lakini wakakosa kuyaelewa. (Yoh 14:26) Pia roho ya Mungu ingewatangazia “mambo yanayokuja.” Hiyo ingeweza kutia ndani kuwafanya waelewe maana ya kifo na ufufuo wa Yesu, kwa kuwa matukio hayo yalikuwa yangali ni ya wakati ujao na yalikuwa miongoni mwa mambo ambayo wanafunzi wake hawakuyaelewa. (Mt 16:21-23; Lu 24:6-8, 19-27; Yoh 2:19-22; 12:14-16; 20:9) Bila shaka, roho ya Mungu iliwawezesha pia wafuasi wa Kristo watabiri matukio ya wakati ujao. (Mdo 11:28; 20:29, 30; 21:11; 1Ti 4:1-3) Ikiwa ndiyo “roho ya ile kweli,” roho takatifu ya Mungu haingeweza kamwe kuwa chanzo cha kosa bali ingewalinda wafuasi wa Kristo kutokana na uwongo mbalimbali wa kimafundisho. (Linganisha 1Yo 2:27; 4:1-6.) Ingetoa ushahidi juu ya kweli inayomhusu Yesu Kristo. Tangu Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, roho ya Mungu ilitoa ushahidi kwa kuwasaidia wanafunzi wa Yesu waelewe unabii mbalimbali uliothibitisha waziwazi kwamba Yesu alikuwa ni Mwana wa Mungu. Walitolea wengine ushahidi kwa msingi wa unabii huo mbalimbali. (Yoh 15:26, 27; linganisha Mdo 2:14-36; Ro 1:1-4.) Hata hivyo, hata kabla ya Pentekoste, “roho ya ile kweli” ilikuwa imetoa ushahidi juu ya uhakika wa kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu (1Yo 5:5-8), kwa maana ni kupitia roho hii kwamba yesu alitiwa mafuta na kuwezeshwa kufanya matendo yenye nguvu nyingi.—Yoh 1:32-34; 10:37, 38; Mdo 10:38; ona ROHO.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki