Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Pata Furaha Tele Katika Yehova’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Desemba 1
    • “Usiwaonee Wivu”

      3, 4. Kama andiko la Zaburi 37:1 linavyoonyesha, Daudi anatoa shauri gani, na kwa nini inafaa kulifuata leo?

      3 Tunaishi katika “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” nao uovu umeenea sana. Tumeona maneno ya mtume Paulo yakitimia: “Watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.” (2 Timotheo 3:1, 13) Ni rahisi kama nini kuathiriwa na yale yanayoonekana kuwa mafanikio na ufanisi wa watu waovu! Yote hayo yanaweza kutukengeusha, na kutufanya tupoteze mtazamo wetu wa kiroho. Ona jinsi maneno ya kwanza ya Zaburi 37 yanavyotuonyesha hatari iliyopo: “Usijionyeshe umewaka hasira kwa sababu ya watenda-maovu. Usiwaonee wivu wale wanaofanya mambo yasiyo ya uadilifu.”

      4 Kila siku vyombo vya habari ulimwenguni huwa na habari nyingi za matendo ya udhalimu. Wafanyabiashara ambao si waaminifu wanaendelea na shughuli zao kwa uhuru. Wahalifu huwashambulia wasio na uwezo. Wauaji hujificha wasipatikane au hata hawaadhibiwi. Mifano yote hiyo ya upotovu wa haki inaweza kutufanya tukasirike na kukosa kuwa na amani ya akili. Yanayoonekana kuwa mafanikio ya watenda-maovu huenda hata yakafanya tuwe na wivu. Lakini je, kukasirika kwetu kutaboresha hali hiyo? Je, kuonea wivu yale yanayoonekana kuwa mafanikio ya watu waovu kunabadili matokeo yao? Sivyo hata kidogo! Na kwa kweli hakuna haja ya ‘kuwaka hasira.’ Kwa nini?

  • ‘Pata Furaha Tele Katika Yehova’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Desemba 1
    • 6. Tunaweza kujifunza nini kutokana na andiko la Zaburi 37:1, 2?

      6 Basi, je, tuuruhusu ufanisi unaopitilia mbali wa watenda-maovu utuhangaishe? Hili ndilo tunalojifunza katika mistari ya kwanza miwili ya Zaburi 37: Usiruhusu kamwe mafanikio yao yakukengeushe kutoka katika njia ambayo umechagua ya kumtumikia Yehova. Badala yake, endelea kukaza fikira zako katika baraka na miradi ya kiroho.—Methali 23:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki