Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Somo la 25. Dunia inavyoonekana kutoka angani.

      SOMO LA 25

      Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?

      Biblia inasema kwamba maisha ya wanadamu ni ‘mafupi na yamejaa taabu.’ (Ayubu 14:1) Je, Mungu anataka tuwe na maisha kama hayo? Ikiwa sivyo, ana kusudi gani kwa wanadamu? Je, kusudi hilo litatimizwa? Chunguza majibu yenye kufariji yanayopatikana katika Biblia.

      1. Yehova anataka tuishi maisha ya aina gani?

      Yehova anataka tuwe na maisha bora kabisa. Alipowaumba wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa, aliwaweka katika paradiso maridadi, bustani ya Edeni. Kisha “Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha.’” (Mwanzo 1:28) Yehova alitaka wapate watoto, waifanye dunia nzima kuwa paradiso na kuwatunza wanyama. Alikusudia kwamba watu wote wawe na afya kamilifu na waishi milele.

      Ingawa mambo ni tofauti leo,a kusudi la Mungu halijabadilika. (Isaya 46:10, 11) Bado anataka wanadamu watiifu waishi milele katika hali kamilifu.​—Soma Ufunuo 21:3, 4.

      2. Tunawezaje kuwa na maisha yenye kusudi leo?

      Yehova alituumba tukiwa na ‘uhitaji wa kiroho,’ yaani, tamaa ya kumjua na kumwabudu. (Soma Mathayo 5:3-6.) Anataka tuwe na urafiki wa karibu pamoja naye, ‘tutembee katika njia zake zote, tumpende,’ na kumtumikia ‘kwa moyo wetu wote.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12; Zaburi 25:14) Tunapofanya hivyo, tunakuwa na furaha ya kweli hata ingawa tunakabili matatizo. Tunapomwabudu Yehova, maisha yetu yanakuwa na kusudi la kweli kwa sababu tunaishi kulingana na viwango vyake.

      CHIMBA ZAIDI

      Jifunze kuhusu upendo mkubwa ambao Yehova alionyesha alipoumba dunia kwa ajili ya wanadamu na kile ambacho Neno lake linasema kuhusu kusudi la uhai.

      Adamu na Hawa wakitazama bustani maridadi iliyokuwa makao yao yenye mimea na wanyama.

      3. Yehova anataka wanadamu wafurahie maisha yenye kusudi

      Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Kwa Nini Mungu Aliiumba Dunia?​—Kisehemu (1:41)

      • Kwa nini Mungu aliiumba dunia yetu maridadi?

      Soma Mhubiri 3:11, kisha mzungumzie swali hili:

      • Andiko hili linakufundisha nini kumhusu Yehova?

      4. Kusudi la Yehova halijabadilika

      Soma Zaburi 37:11, 29 na Isaya 55:11, kisha mzungumzie swali hili:

      • Tunajuaje kwamba kusudi la Yehova kwa wanadamu halijabadilika?

      A. Nyumba iliyoharibika. Paa limeanguka, madirisha yamevunjika, na bustani imejaa takataka. B. Sasa nyumba hiyo imerekebishwa na bustani imetunzwa vizuri.

      Nyumba iliyoharibika kwa sababu ya kupuuzwa inaweza kurekebishwa. Vivyo hivyo, ingawa wanadamu wamekosa kuitunza dunia, Mungu atairekebisha kwa ajili ya wale wanaompenda

      5. Kumwabudu Yehova hufanya maisha yetu yawe na kusudi la kweli

      Tunapata furaha tunapojua kusudi la uhai. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Nilijifunza Kuhusu Kusudi la Uhai (5:03)

      • Terumi alinufaikaje alipojifunza kusudi la uhai?

      Soma Mhubiri 12:13, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa kuwa Yehova ametufanyia mambo mengi sana, tunawezaje kumwonyesha shukrani?

      HUENDA MTU AKAULIZA: “Maisha yana kusudi gani?”

      • Wewe ungejibuje swali hilo?

      MUHTASARI

      Yehova anataka tufurahie maisha milele katika hali kamilifu hapa duniani. Tunapomwabudu kwa moyo wetu wote, maisha yetu yanakuwa na kusudi hata sasa.

      Ungejibuje?

      • Yehova alikuwa na kusudi gani alipowaumba Adamu na Hawa?

      • Tunajuaje kwamba kusudi la Mungu kwa wanadamu halijabadilika?

      • Unawezaje kupata kusudi la kweli maishani?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Chunguza mambo yanayothibitisha kwamba bustani ya Edeni ilikuwepo.

      “Je, Bustani ya Edeni Ilikuwa Halisi au Ni Hadithi Tu?” (Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2011)

      Chunguza uone kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba dunia itadumu milele.

      “Je, Dunia Itaharibiwa?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Jifunze Biblia inasema nini kuhusu jinsi unavyoweza kupata kusudi maishani.

      “Ni Nini Maana ya Uhai?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Ona jinsi mwanamume aliyefikiri ana kila kitu alivyopata kusudi maishani.

      Sasa Nimepata Kusudi Maishani (3:55)

      a Katika somo linalofuata, utajifunza kwa nini kusudi la Mungu halikutimia.

  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 2. Ni nani wanaotawala pamoja na Yesu?

      Yesu anatawala pamoja na wengine. “Watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa . . . watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:9, 10) Ni watu wangapi watakaotawala pamoja na Kristo? Tangu Yesu alipokuja duniani, mamilioni ya watu wamekuwa wafuasi wake. Lakini watu 144,000 ndio tu wanaoenda mbinguni kutawala pamoja na Yesu. (Soma Ufunuo 14:1-4.) Wakristo wengine wote walio duniani watakuwa raia wa Ufalme huo.​—Zaburi 37:29.

  • Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?

      Tayari Ufalme wa Mungu umeanza kutawala. Hivi karibuni utafanya mabadiliko makubwa duniani. Tutachunguza baadhi ya mambo mazuri ambayo tunatazamia kufurahia chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu.

      1. Ufalme wa Mungu utaletaje amani na haki duniani?

      Yesu, Mfalme wa Ufalme wa Mungu, atawaangamiza watu waovu na serikali zote katika vita vya Har–​Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Wakati huo, ahadi hii ya Biblia itatimizwa kikamili: “Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena.” (Zaburi 37:10) Kupitia Ufalme huo, Yesu atahakikisha kwamba kuna amani na haki duniani pote.​—Soma Isaya 11:4.

      2. Maisha yatakuwaje mapenzi ya Mungu yatakapotimizwa duniani?

      Chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, “waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.” (Zaburi 37:29) Wazia kuishi katika ulimwengu ambao kila mtu ni mwadilifu, watu wote wanampenda Yehova na wanapendana! Watu hawatakuwa wagonjwa tena, na kila mtu ataishi milele.

      3. Ufalme wa Mungu utatimiza nini baada ya waovu kuangamizwa?

      Baada ya waovu kuangamizwa, Yesu atatawala akiwa Mfalme kwa miaka elfu moja. Wakati huo, Yesu na watawala wenzake 144,000 watawasaidia wanadamu walio duniani kuwa wakamilifu na wasio na dhambi. Mwishoni mwa kipindi hicho, dunia itakuwa paradiso maridadi, na watu wote watakuwa na furaha kwa sababu ya kutii sheria za Yehova. Kisha Yesu atamrudishia utawala Yehova Baba yake. Wakati huo, ‘jina la Yehova litakuwa limetakaswa’ kikamili. (Mathayo 6:9, 10) Yehova atakuwa amethibitika kuwa Mtawala mzuri anayewajali raia wake. Kisha Yehova atamwangamiza Shetani, roho waovu, na watu wengine watakaoasi utawala wa Mungu. (Ufunuo 20:7-10) Hali kamilifu zitakazoletwa na Ufalme wa Mungu zitadumu milele.

      CHIMBA ZAIDI

      Chunguza kwa nini tunaweza kuamini kwamba Mungu atatumia Ufalme kutimiza ahadi zote zilizo katika Biblia kuhusu wakati ujao.

      4. Ufalme wa Mungu utakomesha serikali za wanadamu

      “Mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Kupitia Ufalme wake, Yehova ataondoa ukosefu huo wa haki.

      Soma Danieli 2:44 na 2 Wathesalonike 1:6-8, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova na Mwana wake, Yesu, watachukua hatua gani dhidi ya serikali za wanadamu na wale wanaoziunga mkono?

      • Mambo ambayo umejifunza kumhusu Yehova na Yesu yanakuhakikishiaje kwamba watatenda kwa haki na bila upendeleo?

      Yesu Mfalme aliye mbinguni akiitawala dunia.

      5. Yesu ndiye Mfalme bora

      Akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu atafanya mambo mengi ili kuwasaidia raia wake. Onyesha VIDEO ili uone kwamba Yesu amethibitisha anatamani kuwasaidia watu na Mungu amempa nguvu za kufanya hivyo.

      VIDEO: Yesu Alionyesha Mambo Ambayo Ufalme Utatimiza (1:13)

      Yesu alipokuwa duniani, alionyesha mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza. Kati ya baraka zilizoonyeshwa, ni baraka gani unayotazamia kwa hamu? Soma Maandiko yaliyoonyeshwa ili kujifunza mengi kuhusu baraka hizo.

      YESU ALIPOKUWA DUNIANI . . .

      YESU AKIWA MBINGUNI . . .

      • alikuwa na nguvu za kudhibiti hali ya hewa.​—Marko 4:36-41.

      • ataondoa uchafuzi wa mazingira duniani.​—Isaya 35:1, 2.

      • alilisha maelfu ya watu kimuujiza.​—Mathayo 14:17-​21.

      • ataondoa tatizo la njaa ulimwenguni.​—Zaburi 72:16.

      • aliponya watu wenye magonjwa mbalimbali.​—Luka 18:35-43.

      • atahakikisha watu wote wana afya kamilifu.​—Isaya 33:24.

      • aliwafufua watu waliokufa.​—Luka 8:49-55.

      • ataondoa madhara yanayosababishwa na kifo.​—Ufunuo 21:3, 4.

      6. Ufalme wa Mungu utaleta wakati ujao ulio bora

      Ufalme wa Mungu utatimiza kikamili kusudi ambalo Yehova alikuwa nalo mwanzoni kuelekea wanadamu. Wanadamu wataishi milele katika paradiso duniani. Onyesha VIDEO ili uone jinsi Yehova anavyomtumia Mwana wake, Yesu, kutimiza kusudi lake.

      VIDEO: Kionjo cha Wakati Ujao Wenye Kupendeza (4:35)

      Soma Zaburi 145:16, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unahisije kujua kwamba Yehova “[atatosheleza] tamaa ya kila kitu kilicho hai”?

      WATU FULANI HUSEMA: “Ikiwa wanadamu wote watashirikiana, tunaweza kutatua matatizo ulimwenguni.”

      • Ufalme wa Mungu utatatua matatizo gani ambayo serikali za wanadamu zimeshindwa kutatua?

      MUHTASARI

      Ufalme wa Mungu utatimiza malengo yake yote. Utaifanya dunia yote kuwa paradiso iliyojaa watu wema watakaomwabudu Yehova milele.

      Ungejibuje?

      • Ufalme wa Mungu utalitakasaje jina la Yehova?

      • Kwa nini tunaweza kuamini kwamba Ufalme wa Mungu utatimiza ahadi zilizo katika Biblia?

      • Ni jambo gani unalotazamia kwa hamu kati ya mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Jifunze maana ya Har–Magedoni.

      “Vita vya Har–Magedoni Ni Nini?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Chunguza kile kitakachotukia katika kipindi ambacho Yesu alikiita “dhiki kuu.”—Mathayo 24:21.

      “Dhiki Kuu Ni Nini?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Ona jinsi familia zinavyoweza kutafakari pamoja kuhusu baraka za wakati ujao za Ufalme wa Mungu.

      Jiwazie Ukiwa Katika Paradiso (1:50)

      Katika makala “Nilikuwa na Maswali Mengi Yaliyonisumbua,” ona jinsi mwasi wa kisiasa alivyopata majibu ya maswali yaliyokuwa yakimhangaisha.

      “Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2012)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki