-
Mngojee YehovaMnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 15
-
-
◆ 42:1—Mtunga Zaburi alikuwaje “kama ayala aoneavyo shauku mito ya maji”?
Kwa sababu fulani, Mlawi huyo alikuwa uhamishoni. Yeye alijisikia akikosa sana ibada katika patakatifu pa Yehova mpaka akajisikia kama ayala au kulungu wa kike ambaye anawindwa, au mwenye kiu, anayetamani sana kupata maji katika nchi isiyozaa, yenye ukame. ‘Aliona kiu’ au alitamani sana Yehova na pendeleo la kumwabudu Mungu kwenye patakatifu Pake.—Mstari wa 2.
-
-
Mngojee YehovaMnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 15
-
-
Somo Kwetu Sisi: Jambo lililoonwa na mtunga zaburi akiwa uhamishoni linapasa litusukume sisi tuonyeshe uthamini wenye kina kirefu kwa ushirika ambao tunafurahia sasa pamoja na watu wa Yehova. Ikiwa kuwekwa kizuizini kwa sababu ya mateso kunatuzuia kwa muda tusiwe pamoja nao, tunaweza kutafakari juu ya furaha za wakati uliopita katika utumishi mtakatifu na tunapaswa kusali ili tupate uvumilivu huku ‘tukimngojea Mungu’ aturudishe katika ushirika wenye utendaji pamoja na waabudu wake.—Zaburi 42:4, 5, 11; 43:3-5, NW.
-