-
Kaa Karibu Na YehovaMnara wa Mlinzi—1991 | Desemba 15
-
-
1. Ni nini mapenzi ya Yehova kuhusu sala, na mtume Paulo alitoa kitia-moyo gani kuhusu kusali?
YEHOVA ni “Mungu atoaye tumaini” kwa watu wake wote waaminifu. Akiwa “Msikiaji wa sala,” yeye husikiliza sihi zao za kuomba msaada kupata tumaini la shangwe ambalo yeye huweka mbele yao. (Warumi 15:13; Zaburi 65:2, NW) Na kupitia Neno lake, Biblia, yeye huwatia moyo watumishi wake wote wamjie wakati wowote wanaotaka. Yeye yupo sikuzote, akitamani kupokea mahangaiko yao ya ndani kabisa. Kwa hakika, yeye huwatia moyo ‘wadumu katika sala’ na ‘kuomba bila kukoma.’a (Warumi 12:12, NW; 1 Wathesalonike 5:17) Ni mapenzi ya Yehova kwamba Wakristo wote wamwendee katika sala, wakimtolea yote yaliyomo mioyoni mwao na kufanya hivyo katika jina la Mwana wake mpendwa, Yesu Kristo.—Yohana 14:6, 13, 14.
-
-
Kaa Karibu Na YehovaMnara wa Mlinzi—1991 | Desemba 15
-
-
3 Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Naam, Mungu si mwenye fahari nyingi mno wala mwenye kuwa mbali mno asiweze kuyasikia maneno tunayomwambia, ijapokuwa hali yetu ya kibinadamu ya kutokamilika. (Matendo 17:27) Zaidi ya hayo, yeye si mwenye kutojali wala kukosa ufikirio. Mtunga zaburi asema hivi: “Macho ya BWANA [Yehova, NW] huwaelekea wenye haki, na masikio yake hukielekea kilio chao.”—Zaburi 34:15; 1 Petro 3:12.
4. Usikivu wa Yehova kwa sala waweza kutolewa kielezi gani?
4 Yehova hukaribisha sala. Twaweza kulinganisha hilo na mkusanyiko ambapo watu kadhaa wanaongea pamoja. Wewe uko huko ukisikiliza wengine wakiongea. Daraka lako ni lile la mtazamaji. Lakini mtu fulani akugeukia, asema jina lako, na kuelekeza maneno yake kwako. Hilo lavuta usikivu wako kwa njia ya pekee. Vivyo hivyo, Yehova huelekeza usikivu wake kwa watu wake sikuzote, popote wawezapo kuwa. (2 Mambo ya Nyakati 16:9; Mithali 15:3) Kwa hiyo yeye husikia maneno yetu, ikiwa kana kwamba anatutazama kwa njia ya kutulinda na kupendezwa nasi. Hata hivyo, tunapoliita jina la Mungu katika sala, usikivu wake unavutwa, na sasa anakazia fikira zake kwetu katika njia dhahiri. Kwa nguvu zake, Yehova aweza hata kuona na kufahamu maombi ya mtu yasiyosemwa yaliyofichwa katika sehemu za ndani kabisa za moyo na akili yake. Mungu anatuhakikishia kwamba atakaribia wale wote wanaoliita jina lake kwa moyo mweupe na kutafuta kukaa karibu naye.—Zaburi 145:18.
-