Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova, Mfanyi wa Mambo ya Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
    • Wema wa Yehova

      8. Twaweza kuwa na ukaribu gani na Yehova, na yeye ameonyeshaje wema wake?

      8 Daudi atoa ombi jingine lenye kuhisiwa moyoni: “Wewe, Ee Yehova, ni mwema na tayari kusamehe; na fadhili-upendo kwa wale wote wanaokuitia ni nyingi. Sikiliza, Ee Yehova, sala yangu; na uelekezee fikira sauti za haja zangu. Katika siku ya taabu yangu nitakuitia, kwa kuwa utanijibu.” (Zaburi 86:5-7, NW) “Ee Yehova”—tena na tena tunasisi-muliwa na ukaribu wa msemo huo! Huo ni ukaribu uwezao kusitawishwa daima kupitia sala. Daudi alisali hivi pindi nyingine: “Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili [fadhili-upendo, NW] zako, Ee BWANA [Yehova, NW], kwa ajili ya wema wako.” (Zaburi 25:7) Yehova ndiye kielelezo bora kabisa cha wema—kwa kuandaa fidia ya Yesu, kwa kuonyesha rehema kwa watenda dhambi wenye kutubu, na kwa kuwamiminia fadhili-upendo Mashahidi wake waaminifu-washikamanifu na wenye kuthamini.—Zaburi 100:3-5; Malaki 3:10.

  • Yehova, Mfanyi wa Mambo ya Ajabu
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Desemba 15
    • 10. Kitabu cha Zaburi kinatolea fadhili-upendo za Yehova umashuhuri gani?

      10 Kitabu cha Zaburi kinarejezea “fadhili-upendo” za Yehova zaidi ya mara mia moja. Fadhili-upendo hizo kwa hakika ni nyingi! Katika mistari yayo minne ya kwanza, Zaburi ya 118, NW, huwasihi watumishi wa Mungu wamshukuru Yehova, ikirudia mara nne, “kwa sababu fadhili-upendo zake ni kwa wakati usiojulikana.” Zaburi ya 136, NW, hukazia ile sifa yenye kupendekeza ya “fadhili-upendo zake” mara 26. Iwe tunakosea katika njia zipi—na kama vile Yakobo 3:2 lisemavyo, “twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi”—na tuwe tayari kutafuta msamaha wa Yehova, tukiwa na uhakika juu ya rehema na fadhili-upendo zake. Fadhili-upendo zake ni wonyesho wa upendo wake mwaminifu-mshikamanifu kuelekea sisi. Tukiendelea kufanya mapenzi ya Mungu kwa uaminifu-mshikamanifu, yeye ataonyesha upendo wake mwaminifu-mshikamanifu kwa kutuimarisha tukabiliane na kila jaribu.—1 Wakorintho 10:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki