Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/1 uku. 30
  • “Neno Lenye Kusemwa Kwenye Wakati Ule Unaofaa”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Neno Lenye Kusemwa Kwenye Wakati Ule Unaofaa”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/1 uku. 30

“Neno Lenye Kusemwa Kwenye Wakati Ule Unaofaa”

“Kama matofaa ya dhahabu katika vichonge vya fedha ni neno lenye kusemwa kwenye wakati ule unaolifaa,” inasema Mithali 25:11, NW. Manenoyetu yenye kufikiriwa kwa uangalifu, na matendo yetu ya fadhili, yanaweza kujongeza moyo wa mtu mwadilifu katika kufuata kile kijia cha kibali cha Yehova. Jambo fulani ambalo huenda sisi tukawa tumesema au kufanya, hata miaka kadha iliyopita, huenda bado likakumbukwa na mtu mwingine kwa kupendezwa sana. Mathalani, alipokuwa akizuru kundi moja, mwangalizi wa mzunguko mmoja na mke wake walikuwa wageni wa dada mpya-mpya aliyebatizwa. Mke wa mwangalizi wa mzunguko alipeleka kibarua cha kupiga asante ili kuthamini ukaribishaji ulioonyeshwa. Zaidi ya miaka saba baadaye, dada huyo alipokea barua inayofuata:

“Mimi nilihisi nikilazimika kabisa kuandika nikuambie kwamba umekuwa msaada mkubwa kwangu muda wa miaka iliyopita, bila ya wewe kujua jambo hilo hasa. Mimi nilikualika wewe na Jim mje kupata chakula kidogo tu cha mchana, na wewe ukanipelekea kadi nzuri sana ya kupiga asante. Ilikuwa na maneno ya kuchangamsha sana, lakini lile andiko hasa ndilo lililofikia moyo wangu, nami sikulisahau kamwe. Hiyo ilikuwa katika 1976. Kwa kweli ni mimi tu katika jamaa yangu niliyekuwa nikipendezwa na ukweli. Mimi nilijifunza na wasichana wangu na kujaribu kuwa mke mwema. Lakini nyakati fulani nilitaka kung’oka nje, kung’oka nje ya ukweli, kung’oka nje ya madaraka hayo​—kung’oka nje kabisa. Lakini andiko lile ambalo wewe uliniandikia likiwa likivuta-vuta moyo wangu, nami nikawa nikijiambia, ‘Mimi ni mbinafsi kama nini kwa kutaka kufanya hivyo,’ nikawa nikiendelea kusonga mbele.

“Hakuna jambo hata moja katika miaka yote hiyo minane lililoniathiri mimi kwa kadiri hiyo, nami nilitaka kukuambia hivyo. Zaidi ya andiko hilo, mimi niliona lilikuwa jambo zuri sana kwamba mtu mwenye shughuli nyingi kama wewe ulichukua fursa ya kunishukuru mimi kwa kufanya jambo ambalo ninapaswa kuwa nikilifanya.

“Oh, ndiyo—andiko lenyewe ni 2 Yohana 8.

“Sandra”

Leo, mume wa Sandra ni mtu aliyebatizwa na anajiunga naye akiwa mhubiri wa zile habari njema. Mmoja wa binti zao wawili ni painia wa kawaida, na binti yule mwingine amekuwa akifanya upainia-msaidizi tangu alipohitimu majuzi kutoka shule ya sekondari.

Mwishowe, 2 Yohana 8, NW inasema nini? “Tazameni kwa hadhari kwa ajili yenu wenyewe, kwamba ninyi msipoteze yale mambo ambayo sisi tumefanya kazi kuyatokeza, bali kwamba ninyi mpate kuwa na thawabu kamili.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki