Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vijana—Sehemu Yenu Katika Jamaa Yenye Furaha, Yenye Umoja
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Novemba 1
    • 10, 11. (a) Kulingana na Mithali 27:19, ni jambo gani linaloweza kuongezea uchangamshi wa jamaa ya Kikristo? (b) Vijana wanaweza kutumiaje mstari huo?

      10 Kufungulia wazazi wako maoni yako ya ndani kunajenga hali ya kupashana habari za moyoni. Unaposema kwa njia tulivu yenye heshima, wazazi wanaweza kuhisi mambo yaliyo katika moyo wako. (Mithali 29:11) Unaona pia sifa zilizo katika mioyo yao. Maongezi hayo kati yenu wawili ya kusemezana waziwazi na kuhurumiana yanakusaidia wewe uujue moyo wako mwenyewe vizuri. Andiko la Mithali 27:19 linasema hivi: “Kama uso ufananavyo na uso [kama vile umbo la kitu linavyoonekana mara ya pili kwa kurudishwa na mwangaza], kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.”a Sawa na vile wewe unavyoona umbo la uso wako lenye kurudishwa na mwangaza katika kidimbwi cha maji matulivu, ndivyo kwa kupashana na wazazi wako habari zilizo moyoni unaweza kuona kwamba maoni yao ya moyoni na makusudio si tofauti sana na yako mwenyewe. Mbadilishano huo wa maoni unafanyiza kuelewana na kujaliana, na hayo ni mambo yanayohitajiwa sana kwa jamaa yenye uchangamshi.

  • Vijana—Sehemu Yenu Katika Jamaa Yenye Furaha, Yenye Umoja
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Novemba 1
    • a Mwelezaji A. Cohen anasema hivi kuhusu mstari huu: “Katika moyo wa rafiki yetu tunaona tabia yetu wenyewe ikionyeshwa humo jinsi ilivyo. . . . Ni katika uhusiano wa urafiki ulio wa kuelezana mambo wazi na kuhurumiana kwamba tunapata kujijua sisi wenyewe kweli kweli, na kutambua yaliyo ndani yetu. (Mithali, The Soncino Press) Tafsiri ya Biblia iliyofanywa na W. F. Beck inasema hivi kwa sehemu: “Kwa hiyo unaweza kuona sura yako ikionyeshwa katika moyo wa mtu mwingine.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki