-
Mfanye Yehova Kuwa Tumaini LakoMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
18, 19. Biblia inatumia maneno gani kututia moyo tumtumaini Yehova, lakini watu fulani wana maoni gani yasiyofaa kuhusiana na hilo?
18 Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5, 6) Maneno hayo mazuri yanatupa uhakika kama nini! Kwa kweli, hakuna mwingine katika ulimwengu wote ambaye anatumainika zaidi kuliko Baba yetu mpendwa wa mbinguni. Hata hivyo, ingawa ni rahisi kusoma maneno haya katika kitabu cha Mithali, huenda isiwe rahisi kuyatenda.
-
-
Mfanye Yehova Kuwa Tumaini LakoMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
22, 23. (a) Kwa nini tunapaswa kumtumaini Yehova tunapokabili matatizo, na tunawezaje kufanya hivyo? (b) Ni nini kitakachozungumziwa katika makala inayofuata?
22 Hata hivyo, andiko la Mithali 3:6 linaonyesha kwamba tunapaswa ‘kumkiri Yehova katika njia zetu zote,’ si wakati tu tunapokabili hali ngumu. Kwa hiyo maamuzi tunayofanya kila siku yanapaswa kuonyesha kwamba tunamtumaini Yehova. Matatizo yanapotokea, hatupaswi kuvunjika moyo, kushtuka, au kukataa mwongozo wa Yehova kuhusu jinsi ya kushughulikia mambo kwa njia bora zaidi. Tunapaswa kuona matatizo kuwa nafasi ya kutetea enzi kuu ya Yehova, kuchangia kumthibitisha Shetani kuwa mwongo, na kusitawisha utii na sifa nyingine zinazompendeza Yehova.—Waebrania 5:7, 8.
-