-
Kuza Urafiki wa Karibu Pamoja na YehovaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
Mfalme huyo mwenye hekima aendelea kusema hivi: “Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.”—Mithali 3:5, 6.
-
-
Kuza Urafiki wa Karibu Pamoja na YehovaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
Twawezaje ‘kumkiri Yehova katika njia zetu zote’? Mtunga-zaburi aliyepuliziwa asema hivi: “Nitaitafakari kazi yako yote; Nitaziwaza habari za matendo yako.” (Zaburi 77:12) Kwa kuwa Mungu haonekani, ni muhimu kutafakari kazi zake kuu na jinsi alivyowatendea watu wake ili kukuza urafiki wa karibu pamoja naye.
Sala pia ni njia muhimu ya kumkiri Yehova. Mfalme Daudi alimlilia Yehova “mchana kutwa.” (Zaburi 86:3) Mara nyingi Daudi alisali usiku kucha, kama wakati alipokuwa mtoro nyikani. (Zaburi 63:6, 7) ‘Endelezeni sala kila wakati,’ akasihi mtume Paulo. (Waefeso 6:18) Sisi husali mara ngapi? Je, sisi hufurahia kuwasiliana na Mungu kutoka moyoni? Tunapokabili hali ngumu, je, sisi humwomba kwa bidii atusaidie? Je, sisi hutafuta mwongozo wake kwa bidii kabla ya kufanya maamuzi muhimu? Yehova hupendezwa nasi tunaposali kwake kutoka moyoni. Naye atuhakikishia kwamba atasikiliza sala zetu na ‘kunyosha mapito yetu.’
-