-
Je, Uko Tayari Kubatizwa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Shinda mambo yanayoweza kukuzuia kubatizwa
Tunapoamua kujiweka wakfu na kubatizwa, sisi sote hukabili changamoto. Ili kuona mfano, onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Katika video hiyo, Narangerel alihitaji kushinda vizuizi gani ili aanze kumtumikia Yehova?
Kumpenda Yehova kulimsaidiaje kushinda vizuizi hivyo?
Soma Methali 29:25 na 2 Timotheo 1:7, kisha mzungumzie swali hili:
Tutapata wapi ujasiri wa kushinda vizuizi?
-
-
Unaweza Kuvumilia MatesoFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
Sasa ndio wakati wa kujifunza kumtegemea Yehova kabisa. Tenga muda kila siku ili kusali kwake na kusoma Neno lake. Hudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. Kufanya mambo hayo kutakupatia nguvu unazohitaji ili ukabili mateso kwa ujasiri, hata kama yanatoka kwa watu wa familia yako. Mtume Paulo, ambaye aliteswa mara nyingi, aliandika hivi: “Yehova ni msaidizi wangu; sitaogopa.”—Waebrania 13:6.
Tunaweza pia kuimarisha ujasiri wetu kwa kuhubiri kwa ukawaida. Tunapohubiri tunajifunza kumtegemea Yehova na kuepuka mtego wa kuwaogopa wanadamu. (Methali 29:25) Ukisitawisha ujasiri wa kuhubiri sasa, utakuwa tayari kuendelea kuhubiri hata ikiwa serikali itajaribu kutuzuia kuhubiri.—1 Wathesalonike 2:2.
-