-
Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo la Kiadili la Kuwa MaskiniMnara wa Mlinzi—1990 | Novemba 15
-
-
Leo, walio wengi wa maskini wa ulimwengu ni wale wapatwao na hali wasizoweza kudhibiti—labda ukosefu wa elimu, uchumi wenye kuzorota katika eneo la kwao, au msukosuko wa kisiasa. Wengi hutoa jasho kuanzia mapema asubuhi hadi usiku sana na kuchakura riziki kidogo tu. Hivyo huenda fursa za kupata fedha kwa njia isiyofuata haki zikaonekana kuwa zenye kuvutia, hata zenye kuhitajiwa kabisa. Kwani, huenda watu fulani wakasababu kwamba Biblia hutetea kuacha maadili pindi kwa pindi! Ingawaje, hiyo husema hivi: “Watu hawamdharau mwivi, akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa.” Na mwanamume mmoja mwenye hekima alisali hivi: ‘Nisije nikawa maskini sana nikaiba.’—Mithali 6:30; 30:8, 9.
-
-
Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo la Kiadili la Kuwa MaskiniMnara wa Mlinzi—1990 | Novemba 15
-
-
Lakini namna gani sala ya huyo mwanamume mwenye hekima? Yeye aliomba kwamba asiweze kuja kwenye umaskini na ‘kuiba na kulitaja bure jina la Mungu wake.’ (Mithali 30:9) Ndiyo, ukosefu wa kufuata haki kwa upande wa mtu adaiye kutumikia Yehova waweza kuleta suto juu ya jina la Mungu na juu ya kundi la watu Wake. Mtume Paulo aliandika hivi: “Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?” Kama watu fulani wenye kudai kuwa Wakristo wangeiba, hiyo ingeweza kusababisha ‘jina la Mungu litukanwe katika Mataifa.’—Warumi 2:21, 24.
-