-
Kuelewa Kusudi la NidhamuMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Hata hivyo, Biblia ina maoni tofauti kuhusu nidhamu. Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika: “Ewe mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova.” (Mithali 3:11, NW) Maneno hayo hayamaanishi nidhamu kwa ujumla, bali “nidhamu ya Yehova,” yaani, nidhamu inayotegemea kanuni za juu za Mungu. Nidhamu hiyo tu ndiyo yenye matokeo, yenye kunufaisha kiroho, na hata yenye kupendeza. Tofauti na hilo, mara nyingi nidhamu inayotegemea maoni ya wanadamu ambayo inapingana na kanuni za juu za Yehova huwa kali na yenye kudhuru. Jambo hilo linaonyesha kwa nini wengi wana maoni yasiyofaa kuhusu nidhamu.
Kwa nini tunahimizwa tukubali nidhamu ya Yehova? Katika Maandiko, nidhamu ya Mungu inafafanuliwa kuwa wonyesho wa upendo wa Mungu kwa ajili ya wanadamu ambao ni viumbe vyake. Kwa hiyo, Sulemani aliendelea kusema: “Yeye ambaye Yehova anampenda, humkaripia, kama vile baba anavyomkaripia mwana anayemfurahia.”—Mithali 3:12, NW.
Kuna Tofauti Gani Kati ya Nidhamu na Adhabu?
Nidhamu inayotajwa katika Biblia inatia ndani mambo mengi—mwongozo, maagizo, mafundisho, karipio, rekebisho, na hata adhabu. Hata hivyo, katika kila kisa, nidhamu ya Yehova hutolewa kwa upendo, na lengo lake huwa ni kumnufaisha mtu anayepewa nidhamu. Nidhamu ambayo Yehova hutoa ili kurekebisha, haitolewi kamwe kwa kusudi la kuadhibu tu.
-
-
Kuelewa Kusudi la NidhamuMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
-
-
Ni katika maana gani adhabu hiyo ‘iliweka kiolezo kwa watu wasiomwogopa Mungu juu ya mambo yajayo’? Katika barua yake kwa Wathesalonike, Paulo anataja siku zetu kuwa wakati ambao Mungu, kupitia Mwana wake Yesu Kristo, ataleta “kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema.” Paulo anaongeza kusema: “Hawahawa watapatwa na adhabu ya kihukumu ya uharibifu udumuo milele.” (2 Wathesalonike 1:8, 9) Ni wazi kwamba adhabu hiyo haikukusudiwa kufundisha wala kurekebisha wenye kuipokea. Hata hivyo, Yehova anapowasihi waabudu wake waikubali nidhamu yake, yeye hamaanishi wakubali adhabu ya watenda dhambi wasiotubu.
Ni jambo la maana kutambua kwamba Biblia haimtaji Yehova kuwa mtoa-adhabu tu. Badala yake, mara nyingi inamtaja kuwa mwalimu mwenye upendo na mfundishaji mwenye subira. (Ayubu 36:22; Zaburi 71:17; Isaya 54:13) Naam, nidhamu ya Mungu inayotolewa kwa kusudi la kurekebisha, sikuzote huambatana na upendo na subira. Wakristo wanapoelewa kusudi la nidhamu, wataweza kuikubali na kuitoa wakiwa na mtazamo unaofaa.
-