Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 5/15 uku. 32
  • Kwa Nini ‘Umwendee Chungu’?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini ‘Umwendee Chungu’?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 5/15 uku. 32

Kwa Nini ‘Umwendee Chungu’?

MFALME Sulemani mwenye hekima wa Israeli wa kale alitoa shauri hili: “Mwendee chungu.” Kwa nini alisema hivyo? na tunaweza kujifunza nini kutoka kwa chungu?

Sulemani aliongeza hivi: “Zitafakari njia [za chungu] ukapate hekima. Kwa maana yeye hana akida, wala msimamizi, wala mkuu, lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.” (Mithali 6:6-8) Maneno hayo ya zamani za kale huonyesha kweli zilizovumbuliwa na wataalamu wa asili wa ki-siku-hizi.

Yule mtunga mithali Aguri aonyesha kwamba chungu ni “wenye hekima kisilika.” (Mithali 30:24, 25, NW) Bila shaka, hekima yao si tokeo la kusababu kiakili bali inatokana na zile silika ambazo Muumba amewapa. Kwa kielelezo, kwa sababu ya silika, chungu hukusanya chakula chao kwa wakati ufaao.

Chungu hufuata utaratibu vizuri ajabu. Wakiwa wafanyakazi wenzi wanaoshirikiana kwa njia ya ajabu na walio macho, wao husaidia chungu waliojeruhiwa au wale waliochoka kurudi kwenye kiota. Wao hutayarishia wakati ujao kisilika na kufanya kila jambo linalowezekana ili kutimiza kazi zao.

Mwendo wa asili wa chungu hudokeza kwamba wanadamu wanapaswa kupanga kimbele na kuwa wafanyakazi wenye bidii. Hilo latumika shuleni, kazini, na katika utendaji mbalimbali wa kiroho. Kama vile chungu hufaidika kutokana na bidii yake, ndivyo Mungu anavyotaka wanadamu ‘wajiburudishe kwa mema katika kazi yao yote.’ (Mhubiri 3:13, 22; 5:18) Kama vile chungu wenye shughuli nyingi, Wakristo wa kweli hutimiza kikamili kazi ya siku nzima. Wao hufanya ‘lolote mkono wao utakalolipata kulifanya,’ si kwa sababu msimamizi anawatazama, bali kwa sababu wanafuata yaliyo ya haki na wana tamaa ya kuwa wafanyakazi wenye bidii, walio na faida.—Mhubiri 9:10; linganisha Mithali 6:9-11; ona pia Tito 2:9, 10.

Kwa kweli, sisi tutakuwa na furaha, ‘tukimwendea chungu’ na kutumia yale tunayojifunza kutoka kwake. Na furaha iliyo kubwa zaidi itakuwa yetu tukifanya kwa bidii-nyendelevu mapenzi ya Yehova Mungu, kama yanavyofunuliwa katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki