-
“Uzishike Amri Zangu Ukaishi”Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
“Huyo akafuatana naye mara hiyo,” aripoti Solomoni, “kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu; hata mshale umchome maini; kama ndege aendaye haraka mtegoni; wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.”—Mithali 7:22, 23.
Kijana huyo ashindwa kukataa mwaliko huo. Huku akipuuza busara, anamfuata ‘kama ng’ombe aendaye machinjoni.’ Kama vile mtu aliyefungwa pingu miguuni asivyoweza kutoroka adhabu yake, ndivyo kijana huyo anavyovutwa kwenye dhambi. Haoni hatari yote iliyopo mpaka “mshale umchome maini,” yaani mpaka apate kidonda kinachoweza kumwua. Kifo hicho chaweza kuwa cha asili katika maana ya kwamba anaweza kupatwa na maradhi yanayoambukizwa kingono ambayo huua.b Kidonda hicho chaweza pia kuharibu kabisa hali yake ya kiroho; ‘chahusisha nafsi yake mwenyewe.’ Yeye mwenyewe na maisha yake yameathiriwa sana, na amemkosea sana Mungu. Hivyo anakimbia katika kifo kama ndege aendaye mtegoni!
-
-
“Uzishike Amri Zangu Ukaishi”Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
b Maradhi fulani yanayoambukizwa kingono huharibu ini. Kwa mfano, kaswende inapokomaa, hufanya ini lilemewe na bakteria. Navyo vijidudu vinavyosababisha kisonono vyaweza kufanya ini livimbe.
-