Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Bwana Huwapa Watu Hekima”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • Kwa maneno yaliyo kama ya baba mwenye upendo, Mfalme Solomoni wa Israeli la kale ambaye alikuwa mwenye hekima, asema: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara [“uelewevu,” “NW”], na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, na kuutafutia kama hazina iliyositirika; ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, na kupata kumjua Mungu.”—Mithali 2:1-5.

      Je, unatambua ni nani aliye na daraka la kutafuta hekima? Katika mistari hiyo, usemi “uki-” waonekana mara tatu. Ni wazi kwamba kila mmoja wetu ana daraka la kutafuta hekima na sifa nyingine zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu. Lakini, kwanza, twahitaji ‘kukubali’ na “kuyaweka akiba” akilini maneno ya hekima yaliyorekodiwa katika Maandiko. Ili kufanya hivyo, twahitaji kujifunza Biblia.

  • “Bwana Huwapa Watu Hekima”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • Neno “uki-” ambalo limerudiwa-rudiwa katika mafungu ya kwanza katika sura ya pili ya Mithali linafuatwa na semi kama “kubali,” “kuweka akiba,” “kuita,” “kutafuta,” “kutafutia.” Kwa nini mwandishi anatumia semi hizi zenye kukazia maana zaidi na zaidi? Kitabu kimoja cha marejezo chasema: “[Hapa] huyo mwenye hekima anakazia uhitaji wa kujitahidi kutafuta hekima.” Naam, ni lazima tujitahidi kutafuta hekima na sifa zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki