-
Endelea Kunufaika kwa Kumwogopa MunguMnara wa Mlinzi (Funzo)—2023 | Juni
-
-
6. Tutazungumzia wanawake gani wawili wa mfano?
6 Acheni tuchunguze Methali sura ya 9, ambayo inalinganisha hekima na upumbavu, na wanawake wawili wa mfano. (Linganisha Waroma 5:14; Wagalatia 4:24.) Tunapofanya hivyo, kumbuka kwamba ulimwengu wa Shetani unakazia sana uasherati na ponografia. (Efe. 4:19) Basi, ni jambo muhimu tuendelee kusitawisha woga kumwelekea Mungu na kujiepusha na uovu. (Met. 16:6) Hivyo, sisi sote iwe ni wanaume au wanawake tunaweza kunufaika kutokana na sura hiyo. Kila mmoja wa wanawake hao wawili anatoa mwaliko kwa wajinga, yaani, wale “wasio na busara.” Ni kana kwamba kila mwanamke anasema hivi, ‘Karibu nyumbani kwangu tule chakula.’ (Met. 9:1, 5, 6, 13, 16, 17) Lakini kila mwaliko una matokeo yaliyo tofauti sana.
-
-
Endelea Kunufaika kwa Kumwogopa MunguMnara wa Mlinzi (Funzo)—2023 | Juni
-
-
“Mwanamke mpumbavu” anatoa mwaliko unaoweza kusababisha matokeo mabaya (Tazama fungu la 7)
7. Kulingana na Methali 9:13-18, mwaliko wa mwanamke mpumbavu una matokeo gani? (Tazama pia picha.)
7 Fikiria mwaliko unaotoka kwa “mwanamke mpumbavu.” (Soma Methali 9:13-18.) Kwa ujasiri na kwa sauti kubwa anawaambia hivi wale wasio na busara, ‘Njooni hapa’ mle chakula. Wanapatwa na matokeo gani? “Wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo.” Huenda ukakumbuka lugha kama hiyo ya mfano inayotumiwa mwanzoni mwa kitabu cha Methali. Tunaonywa kuhusu “mwanamke aliyepotoka” na “mwanamke mwasherati.” Tunaambiwa hivi: “Nyumba yake huzama katika kifo.” (Met. 2:11-19) Methali 5:3-10 inatoa onyo kuhusu ‘mwanamke mwingine aliyepotoka’ ambaye “miguu yake hushuka kwenye kifo.”
8. Tunapaswa kufanya uamuzi gani?
8 Wale wanaosikia sauti ya “mwanamke mpumbavu” wanahitaji kufanya uamuzi huu: Je, watakubali mwaliko wake au wataukataa? Huenda sisi pia tukahitaji kufanya uamuzi kama huo. Tutafanya nini ikiwa tutashawishiwa kufanya uasherati au kutazama picha au video za ponografia kwenye Intaneti?
-