Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Endelea Kunufaika kwa Kumwogopa Mungu
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2023 | Juni
    • Mwanamke kahaba wa nyakati za kale, amesimama kwenye mlango wa nyumba yake akimwalika mwanamume aingie ndani.

      “Mwanamke mpumbavu” anatoa mwaliko unaoweza kusababisha matokeo mabaya (Tazama fungu la 7)

      7. Kulingana na Methali 9:13-18, mwaliko wa mwanamke mpumbavu una matokeo gani? (Tazama pia picha.)

      7 Fikiria mwaliko unaotoka kwa “mwanamke mpumbavu.” (Soma Methali 9:13-18.) Kwa ujasiri na kwa sauti kubwa anawaambia hivi wale wasio na busara, ‘Njooni hapa’ mle chakula. Wanapatwa na matokeo gani? “Wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo.” Huenda ukakumbuka lugha kama hiyo ya mfano inayotumiwa mwanzoni mwa kitabu cha Methali. Tunaonywa kuhusu “mwanamke aliyepotoka” na “mwanamke mwasherati.” Tunaambiwa hivi: “Nyumba yake huzama katika kifo.” (Met. 2:11-19) Methali 5:3-10 inatoa onyo kuhusu ‘mwanamke mwingine aliyepotoka’ ambaye “miguu yake hushuka kwenye kifo.”

  • Endelea Kunufaika kwa Kumwogopa Mungu
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2023 | Juni
    • 10 Uasherati unaweza kusababisha aibu, kujihisi kwamba hufai, mimba zisizotakikana, na kuvunjika kwa familia. Ni wazi kwamba ni jambo la hekima kuepuka “nyumba” ya mwanamke mpumbavu na chakula chake. Mbali na kupoteza kibali cha Yehova, wengi wanaofanya uasherati hupatwa na magonjwa ambayo yanasababisha kifo cha mapema. (Met. 7:23, 26) Methali 9:18 inamalizia kwa kusema hivi: “Wageni wake wamo katika vina vya kaburi.” Basi, kwa nini watu wengi hukubali mwaliko wa mwanamke huyo unaoongoza kwenye msiba?​—Met. 9:13-18.

  • Endelea Kunufaika kwa Kumwogopa Mungu
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2023 | Juni
    • Mwanamke wa nyakati za kale za Israeli, anawaalika wenzi wa ndoa nyumbani kwake ili wale karamu ya chakula chenye afya kinachopendeza ambacho kimeandaliwa mbele yao.

      Kukubali mwaliko wa “hekima ya kweli” kutatusaidia kuishi milele (Tazama fungu la 17 na 18)

      17-18. Wale wanaokubali mwaliko wa “hekima ya kweli” wanafurahia baraka gani, na wanatazamia nini wakati ujao? (Tazama pia picha.)

      17 Yehova anatumia mifano ya wanawake hao wawili, ili kutuonyesha jinsi tunavyoweza kuwa na wakati ujao wenye furaha. Wale wanaokubali mwaliko unaotolewa kwa sauti kubwa na “mwanamke mpumbavu,” wanakazia fikira kujifurahisha kupitia ukosefu wa maadili kisiri. Lakini hawatambui kwamba mambo wanayofanya yataathiri wakati wao ujao. Matendo yao yatawaongoza katika “vina vya Kaburi.”​—Met. 9:13, 17, 18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki