-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Kwa maneno yaliyo kama ya baba mwenye upendo, Mfalme Solomoni wa Israeli la kale ambaye alikuwa mwenye hekima, asema: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara [“uelewevu,” “NW”], na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, na kuutafutia kama hazina iliyositirika; ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, na kupata kumjua Mungu.”—Mithali 2:1-5.
-
-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Kuzingatia hekima kwahusisha kujifunza ufahamu na uelewevu. Kwa mujibu wa Webster’s Revised Unabridged Dictionary, ufahamu ni “nguvu au uwezo unaowezesha akili kupambanua mambo.” Ufahamu wa kimungu ni uwezo wa kupambanua mema na mabaya, kisha kuchagua mwenendo ufaao. ‘Tusipoielekeza mioyo’ yetu ipate ufahamu au tusipokuwa na hamu ya kujipatia ufahamu huo, tunawezaje kukaa katika ‘barabara iongozayo kuingia katika uhai’? (Mathayo 7:14; linganisha Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.) Kujifunza na kutumia Neno la Mungu hutupa ufahamu.
Tunawezaje ‘kuita uelewevu’—uwezo wa kutambua jinsi sehemu mbalimbali za habari fulani zinavyohusiana kwa jumla? Bila shaka, umri na uzoefu ni mambo yawezayo kutusaidia tusitawishe uelewevu zaidi—lakini nyakati nyingi haiwi hivyo. (Ayubu 12:12; 32:6-12) “Ninao ufahamu kuliko wazee,” akasema mtunga-zaburi, “kwa kuwa nimeyashika mausia yako [Yehova].” Pia aliimba hivi: “Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga [“asiye na uzoefu,” NW].” (Zaburi 119:100, 130) Yehova ndiye “mzee wa siku,” naye ana uelewevu mkubwa zaidi kushinda binadamu yeyote. (Danieli 7:13) Mungu anaweza kumpa uelewevu mtu asiye na uzoefu, akimwezesha kuwa na uelewevu mwingi zaidi kushinda wazee. Hivyo, yatupasa kujitahidi kujifunza na kutumia Neno la Mungu, Biblia.
Neno “uki-” ambalo limerudiwa-rudiwa katika mafungu ya kwanza katika sura ya pili ya Mithali linafuatwa na semi kama “kubali,” “kuweka akiba,” “kuita,” “kutafuta,” “kutafutia.” Kwa nini mwandishi anatumia semi hizi zenye kukazia maana zaidi na zaidi? Kitabu kimoja cha marejezo chasema: “[Hapa] huyo mwenye hekima anakazia uhitaji wa kujitahidi kutafuta hekima.” Naam, ni lazima tujitahidi kutafuta hekima na sifa zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu.
-