-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Kwa maneno yaliyo kama ya baba mwenye upendo, Mfalme Solomoni wa Israeli la kale ambaye alikuwa mwenye hekima, asema: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara [“uelewevu,” “NW”], na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, na kuutafutia kama hazina iliyositirika; ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, na kupata kumjua Mungu.”—Mithali 2:1-5.
-
-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Neno “uki-” ambalo limerudiwa-rudiwa katika mafungu ya kwanza katika sura ya pili ya Mithali linafuatwa na semi kama “kubali,” “kuweka akiba,” “kuita,” “kutafuta,” “kutafutia.” Kwa nini mwandishi anatumia semi hizi zenye kukazia maana zaidi na zaidi? Kitabu kimoja cha marejezo chasema: “[Hapa] huyo mwenye hekima anakazia uhitaji wa kujitahidi kutafuta hekima.” Naam, ni lazima tujitahidi kutafuta hekima na sifa zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu.
Je, Utajitahidi?
Jambo muhimu katika ufuatiaji wa hekima ni funzo la bidii la Biblia. Lakini funzo hilo lapaswa kutia ndani mengi zaidi ya kusoma tu ili kupata habari. Sehemu muhimu katika kujifunza Maandiko ni kupanga kutafakari yale tunayosoma. Kupata hekima na ufahamu huhusisha kutafakari jinsi tuwezavyo kutumia yale tunayojifunza katika kutatua matatizo na kufanya maamuzi. Kujipatia uelewevu kwahitaji kutafakari jinsi habari mpya inavyopatana na yale ambayo tayari tunajua. Ni nani awezaye kukanusha kwamba kujifunza Biblia kwa makini hivyo kunahitaji wakati na jitihada nyingi? Wakati na nguvu unazotumia zatoshana na zile zinazotumiwa ‘kutafuta fedha na kutafutia hazina iliyositirika.’ Je, utajitahidi inavyohitajiwa? Je, ‘utanunua kabisa wakati’ ili kufanya hivyo?—Waefeso 5:15, 16.
-