-
Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
KWA NINI TUNAPASWA KUWA WAANGALIFU KUHUSU YALE TUNAYOSEMA?
4, 5. Methali fulani za Biblia zinafafanua jinsi gani madhara ambayo yanaweza kusababishwa na maneno?
4 Sababu moja muhimu ya kuwa waangalifu kuhusu yale tunayosema ni kwamba maneno yana nguvu. Andiko la Methali 15:4 linasema: “Utulivu wa ulimi ni mti wa uzima, lakini upotovu wake humaanisha kuvunjika katika roho.”a Kama vile maji yanavyoupa uhai mti ulionyauka, ndivyo maneno yanayosemwa kwa utulivu yanavyoweza kuiburudisha roho ya wale wanaoyasikia. Kwa upande mwingine, maneno yaliyopotoka ya ulimi mpotovu yanaweza kuwafanya wengine wavunjike katika roho. Kwa kweli, maneno tunayosema yana nguvu za kuumiza au kuponya.—Methali 18:21.
-
-
Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
a Neno la Kiebrania linalotafsiriwa ‘potovu’ kwenye Methali 15:4 linaweza pia kumaanisha “kombo,” au “kaidi.”
-