Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Iweni Waigaji wa Mungu” Mnapotumia Uwezo
    Mkaribie Yehova
    • 10. (a) Mungu amewapa wazazi mamlaka gani? (b) Neno “nidhamu” linamaanisha nini, na inapasa kutolewaje? (Ona pia kielezi-chini.)

      10 Wazazi pia wamepewa mamlaka na Mungu. Biblia inashauri hivi: “Akina baba, msiwe mkiwasumbua watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.” (Waefeso 6:4) Katika Biblia, neno “nidhamu” linaweza kumaanisha “malezi, mazoezi, mafundisho.” Watoto wanahitaji nidhamu; wanafurahi na kufanikiwa wanapopewa maagizo yaliyo wazi, na wanapowekewa mipaka na vizuizi. Kulingana na Biblia, nidhamu au mafundisho huhusisha upendo. (Mithali 13:24) Kwa hiyo, “fimbo ya adhabu” haipaswi kamwe kuwaumiza watoto kihisia-moyo au kimwili.a (Mithali 22:15; 29:15) Mzazi anayetoa nidhamu kwa ukali bila upendo anatumia vibaya mamlaka yake. Kufanya hivyo kunaweza kumvunja moyo mtoto. (Wakolosai 3:21) Kwa upande mwingine, kutoa nidhamu kwa usawaziko na kwa njia ifaayo kunawathibitishia watoto kwamba wazazi wanawapenda na wanapendezwa na utu wanaositawisha.

  • “Iweni Waigaji wa Mungu” Mnapotumia Uwezo
    Mkaribie Yehova
    • a Katika nyakati za Biblia, neno la Kiebrania linalotafsiriwa “fimbo” lilimaanisha kijiti au gongo kama lile lililotumiwa na mchungaji kuwaongoza kondoo. (Zaburi 23:4) Vivyo hivyo, “fimbo” ya mamlaka ya wazazi inaonyesha mwongozo wa upendo, wala si adhabu kali au ya kikatili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki