Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Chenye Kutumika Kwa Maisha Ya Kisasa
    Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
    • Afya ya mtu ya kimwili huathiriwa mara nyingi na hali yake ya akilini na afya ya kihisia-moyo. Mathalani, uchunguzi mbalimbali wa kisayansi umethibitisha matokeo yenye kudhuru ya hasira. “Mwingi wa uthibitisho unaopatikana hudokeza kwamba watu wenye uhasama wamo katika hatari zaidi ya kupatwa na maradhi ya moyo (pamoja na magonjwa mengine) kwa sababu mbalimbali, kutia ndani kuwa na marafiki wachache zaidi, ongezeko la matokeo ya kimwili wanapokasirishwa, na kujihusisha zaidi katika mazoea yenye kuudhuru mwili,” wasema Dakt. Redford Williams, Mkurugenzi wa Utafiti wa Tabia kwenye Duke University Medical Center, na mkewe, Virginia Williams, katika kitabu chao Anger Kills.13

      Maelfu ya miaka kabla ya uchunguzi huo wa kisayansi, Biblia, katika maneno sahili lakini ya wazi, ilihusianisha hali yetu ya kihisia-moyo na afya yetu ya kimwili hivi: “Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; bali husuda ni ubovu wa mifupa.” (Mithali 14:30; 17:22) Kwa hekima, Biblia ilishauri hivi: “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu,” na “Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako.”—Zaburi 37:8; Mhubiri 7:9.

  • Kitabu Chenye Kutumika Kwa Maisha Ya Kisasa
    Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
    • “Usiwe mwepesi wa kuonyesha uchungu wa moyo; kwa kuwa uchungu wa moyo hudumishwa na wapumbavu.” (Mhubiri 7:9, The New English Bible) Mara nyingi hisia-moyo hutangulia matendo. Mtu aliye mwepesi wa kuudhika ni mpumbavu, kwa maana mwendo wake huenda ukaongoza kwenye maneno au matendo ya kutofikiri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki