-
Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?Amkeni!—2007 | Juni
-
-
Maoni ya Biblia
Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?
BIBLIA inasema: “Pesa ni ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Kwa kuwa zinaweza kununua chakula, mavazi, na nyumba, pesa ni ulinzi dhidi ya umaskini. Ndiyo, pesa zinaweza kununua mali zozote zile. Mhubiri 10:19 inasema hivi: “Pesa ndizo hutokeza jibu katika mambo yote.”
-
-
Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?Amkeni!—2007 | Juni
-
-
Kitu Kilicho Bora Kuliko Pesa
Alipotaja kwamba pesa ni ulinzi, Mfalme Sulemani aliongeza kwamba “hekima ni ulinzi,” kwa sababu ‘inawahifadhi hai waliyo nayo.’ (Mhubiri 7:12) Alimaanisha nini? Sulemani alikuwa akizungumzia hekima inayotegemea ujuzi sahihi wa Maandiko na kumwogopa Mungu kwa njia inayofaa. Hekima hiyo inayotoka kwa Mungu ambayo ni bora kuliko pesa, inaweza kumsaidia mtu aepuke kifo cha mapema na matatizo mengi maishani. Pia, sawa na taji, hekima ya kweli huwatukuza walio nayo na kuwaletea heshima. (Methali 2:10-22; 4:5-9) Na kwa sababu inawezesha mtu kupata kibali cha Mungu, inaitwa “mti wa uzima.”—Methali 3:18.
Wale wanaotaka kikweli hekima hiyo na wale wanaotaka kuitafuta, hutambua kwamba inaweza kupatikana. “Mwanangu, ikiwa . . . utaita uelewaji na kupaaza sauti yako uite utambuzi, ikiwa utaendelea kuutafuta kama fedha, na kuendelea kuutafuta kama hazina zilizofichika, ndipo utakapoelewa kumwogopa Yehova, nawe utapata kumjua Mungu. Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima; kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.”—Methali 2:1-6.
-