Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kufanya Maamuzi Mazuri
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Heshimu dhamiri za watu wengine

      Maamuzi yetu hutofautiana na maamuzi ya watu wengine. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu dhamiri za watu wengine? Fikiria hali mbili zinazofuata:

      Hali ya 1: Dada anayependa kujipamba anahamia kutaniko ambalo dada wengi wanakwazika wanapoona watu wakijipamba.

      Soma Waroma 15:1 na 1 Wakorintho 10:23, 24, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, dada huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini unaposhughulika na mtu ambaye dhamiri yake inamkataza kufanya jambo ambalo dhamiri yako inakubali?

      Hali ya 2: Ndugu ambaye anajua kwamba Biblia haikatazi kunywa kileo kwa kiasi, lakini anaamua kutokunywa kileo. Anakaribishwa kwenye tafrija ambapo anaona akina ndugu wakinywa kileo.

      Soma Mhubiri 7:16 na Waroma 14:1, 10, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, ndugu huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini ukimwona mtu anafanya jambo ambalo dhamiri yako inakuzuia kufanya?

      Hatua zinazotusaidia kufanya maamuzi mazuri.

      Mwanamke akisali.

      1. Mwombe Yehova akusaidie kuamua jambo la kufanya.​—Yakobo 1:5.

      Mwanamke huyo akifanya utafiti kwa kutumia Biblia, machapisho yanayotegemea Biblia, na kompyuta.

      2. Fanya utafiti katika Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia ili upate kanuni zinazohusika. Unaweza pia kuzungumza na Wakristo wenye uzoefu.

      Mwanamke huyo akifikiria.

      3. Fikiria matokeo ya uamuzi utakaofanya, yaani, jinsi utakavyoathiri dhamiri yako na dhamiri za watu wengine.

  • Unawezaje Kumfurahisha Yehova Kupitia Mazungumzo Yako?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Sema mambo mazuri kuwahusu wengine

      Tunawezaje kuepuka kusema mambo yanayowaumiza wengine au kusema mambo yasiyo ya fadhili? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Sema ‘Neno Jema kwa Ajili ya Kuwajenga’ Wengine (4:07)

      • Katika video hiyo, kwa nini ndugu huyo alitaka kubadili jinsi alivyozungumza kuhusu wengine?

      • Alifanya nini ili abadili njia yake ya kuzungumza?

      Soma Mhubiri 7:16, kisha mzungumzie swali hili:

      • Tunapaswa kukumbuka nini tunaposhawishiwa kusema mambo yasiyofaa kuhusu mtu mwingine?

      Soma Mhubiri 7:21, 22, kisha mzungumzie swali hili:

      • Mistari hii inawezaje kukusaidia usikasirike mtu anaposema mambo yasiyofaa kukuhusu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki