Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • 12. Kwa maneno yako mwenyewe, unaweza kuelezaje maneno ya Solomoni katika Mhubiri 12:11, 12?

      12 Hata bila mbinu za kisasa za uchapishaji, kulikuwa na vitabu vingi katika siku za Solomoni. Fasihi kama hizo zilipasa kuonwaje? Yeye alisema: “Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoro; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko [“mikusanyo ya maneno,” NW], ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja. Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.”—Mhubiri 12:11, 12.

  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • 14. (a) Hainufaishi “kusoma sana” vitabu vya aina gani? (b) Tunapaswa kuzingatia sana fasihi gani, na kwa nini?

      14 Lakini, kwa nini Solomoni aseme hivyo kuhusu vitabu? Kwa kulinganisha na Neno la Yehova, vitabu vingi sana vya ulimwengu huu vina fikira za wanadamu tu. Vingi vinaonyesha fikira za Shetani Ibilisi. (2 Wakorintho 4:4) Kwa hiyo, hakuna manufaa ya kudumu ya ‘kuvisoma sana’ vitabu hivyo vya kilimwengu. Vingi vya vitabu hivyo hata vinaweza kudhuru kiroho. Kama Solomoni, na tutafakari yale ambayo Neno la Mungu lisemayo kuhusu uhai. Kufanya hivyo kutaimarisha imani yetu na kutufanya tuwe karibu zaidi na Yehova. Kuvisoma sana vitabu vingine au mafundisho mengine kunaweza kutuchosha sana. Hasa kama maandishi hayo yanatokana na kusababu kwa kilimwengu ambako kunahitilafiana na hekima ya kimungu basi hayafai na yanaweza kuharibu imani katika Mungu na makusudi yake. Basi, na tukumbuke kwamba maandishi mengi yenye kunufaisha katika siku za Solomoni na katika siku zetu ni yale yaonyeshayo hekima ya “mchungaji mmoja,” Yehova Mungu. Ameandaa vitabu 66 vya Maandiko Matakatifu, na tunapaswa kuvizingatia sana. Biblia na vichapo vyenye msaada vya ‘mtumwa mwaminifu’ hutuwezesha kupata ‘kumjua Mungu.’—Mithali 2:1-6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki