-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
21. Fafanua ukamilifu wa baraka zitakazokuja.
21 “Juu ya kila mlima mrefu, na juu ya kila kilima kilichoinuka, itakuwapo mito na vijito vya maji.” (Isaya 30:25a)c Isaya atoa mfano unaokazia ukamilifu wa baraka za Yehova. Hakuna upungufu wa maji—kitu chenye thamani kitakachotiririka, siyo katika mabonde tu, bali pia katika kila mlima, “juu ya kila mlima mrefu, na juu ya kila kilima kilichoinuka.” Naam, njaa haitakuwapo. (Zaburi 72:16) Isitoshe, uangalifu wa nabii huyo wageukia hata mambo yaliyo juu kuliko milima. “Nuru ya mwezi itakuwa kama nuru ya jua, na nuru ya jua itaongezeka mara saba, kama nuru ya siku saba, katika siku ile BWANA atakapofunga mapigo ya watu wake, na kuliponya pigo la jeraha yao.” (Isaya 30:26) Huo ni upeo wenye kusisimua kama nini wa unabii huu mtukufu! Utukufu wa Mungu utang’aa katika fahari. Baraka watakazopata waabudu waaminifu wa Mungu zitakuwa nyingi sana—mara saba—kuliko chochote ambacho wamewahi kupata hapo awali.
-
-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
c Andiko la Isaya 30:25b lasema: “Katika siku ya machinjo makuu itakapoanguka minara.” Katika utimizo wa mwanzoni, huenda maneno hayo yarejezea kuanguka kwa Babiloni, uliofungua njia kwa Israeli kufurahia baraka zilizotabiriwa kwenye Isaya 30:18-26. (Ona fungu la 19.) Huenda yakarejezea pia uharibifu kwenye Har–Magedoni, utakaofanya iwezekane kuwe na utimizo mtukufu zaidi wa baraka hizo katika ulimwengu mpya.
-
-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 311]
“Juu ya kila kilima kilichoinuka, itakuwapo mito na vijito vya maji”
-