-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Tofauti na baraka ambazo waaminifu watapata, Yehova atawatenda waovu nini?
22 Sauti ya Isaya yabadilika tena atoapo ujumbe huu. “Tazama” yeye asema, kana kwamba ataka wasikilizaji wake wasikilize kwa makini. “Jina la BWANA linakuja kutoka mbali sana, linawaka kwa hasira yake, kwa moshi mwingi sana unaopaa juu; midomo yake imejaa ghadhabu, na ulimi wake ni moto ulao.” (Isaya 30:27) Hadi sasa, Yehova hajaingilia kati, akiwaruhusu adui za watu wake wafuate mwendo wao wenyewe. Sasa yeye asonga karibu zaidi—kama mvua ya radi—ili kutekeleza hukumu. “Pumzi yake ni kijito kifurikacho, kifikacho hata shingoni, kupepeta mataifa kwa ungo wa ubatili; na lijamu ikoseshayo itakuwa katika taya za watu.” (Isaya 30:28) Adui za watu wa Mungu watazungukwa kwa “kijito kifurikacho,” watatikiswa kijeuri “kwa ungo,” na kuzuiwa kwa “lijamu.” Wataharibiwa.
-
-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 312]
Yehova atakuja “kwa hasira yake, kwa moshi mwingi sana”
-