-
Mfalme na Wakuu WakeUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
5-7. “Wakuu” waliotabiriwa wanatimiza wajibu gani katika kundi la Mungu?
5 Hata hivyo, maadamu ulimwengu wa sasa uliojaa chuki upo, washiriki wa umati mkubwa wahitaji ulinzi. Kwa jumla, “wakuu” ‘wanaotawala kwa haki,’ ndio wanaotoa ulinzi huo. Huo ni mpango bora kama nini! “Wakuu” hao wanafafanuliwa zaidi kwa maneno mazuri ya unabii wa Isaya: “Mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.”—Isaya 32:2.
6 Hivi sasa katika wakati huu wa taabu ya ulimwenguni kote, kuna uhitaji wa “wakuu,” yaani, wazee ‘wanaokazia uangalifu kwa kundi lote,’ wakitunza kondoo za Yehova na kutekeleza haki kupatana na kanuni za Yehova za uadilifu. (Matendo 20:28) Ni lazima “wakuu” hao wawe na sifa zilizo katika 1 Timotheo 3:2-7 na Tito 1:6-9.
7 Katika unabii wake mkubwa unaoeleza “umalizio wa mfumo wa mambo” wenye kujaa taabu, Yesu alisema: “Angalieni kwamba hamwogofishwi.” (Mathayo 24:3-8) Sababu gani hali hatari za ulimwengu wa leo haziwaogofishi wafuasi wa Yesu? Sababu moja ni kwamba “wakuu”—iwe ni watiwa-mafuta au “kondoo wengine”—wanalinda kundi kwa uaminifu-mshikamanifu. (Yohana 10:16) Wao huwatunza ndugu na dada zao bila woga, hata wanapokabiliwa na vitisho kama vita vya ukabila na maangamizi ya jamii nzima-nzima. Katika ulimwengu wenye njaa ya kiroho, wao huhakikisha kwamba nafsi zilizoshuka moyo zimefarijiwa kupitia kweli zinazojenga za Neno la Mungu, Biblia.
8. Ni kwa njia gani Yehova anawazoeza na kuwatumia “wakuu” ambao ni sehemu ya kondoo wengine?
8 Kwa miaka 50 iliyopita, “wakuu” hao wameonekana waziwazi. “Wakuu” walio sehemu ya kondoo wengine wanazoezwa wakiwa jamii ya “mkuu” inayozidi kukua ili baada ya dhiki kubwa, watu wanaostahili miongoni mwao wawe tayari kuteuliwa kutumikia wakiwa wasimamizi katika “dunia mpya.” (Ezekieli 44:2, 3; 2 Petro 3:13) Kwa kuandaa mwelekezo na burudisho la kiroho waongozapo katika utumishi wa Ufalme, wanajithibitisha wenyewe kuwa “kama kivuli cha mwamba mkubwa,” wakililetea kundi kitulizo katika eneo lake la ibada.b
9. Ni hali gani zinazoonyesha kwamba kuna uhitaji wa “wakuu” leo?
9 Katika siku hizi za mwisho zenye hatari za ulimwengu wa Shetani, Wakristo waliojiweka wakfu wahitaji sana ulinzi huo. (2 Timotheo 3:1-5, 13) Pepo kali za mafundisho yasiyo ya kweli na propaganda iliyopotoka zinavuma. Vita mithili ya dhoruba vinaendelea kati ya mataifa na ndani ya mataifa na vilevile kuna mashambulizi ya moja kwa moja dhidi ya waabudu waaminifu wa Yehova Mungu. Katika ulimwengu uliokaushwa na ukame wa kiroho, Wakristo wanahitaji sana vijito vya maji safi ya kweli yasiyoghushiwa ili wakate kiu yao ya kiroho. Yafurahisha kwamba Yehova ameahidi kwamba Mfalme wake anayetawala, kupitia ndugu zake watiwa-mafuta na “wakuu” wanaowasaidia kati ya kondoo wengine, ataandaa kitia-moyo na mwelekezo kwa watu walioshuka na kuvunjika moyo katika kipindi hiki chenye uhitaji. Hivyo basi, Yehova atahakikisha kuwa mambo ya uadilifu na ya haki yamedumu.
-
-
Mfalme na Wakuu WakeUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 333]
Kila ‘mkuu’ ni kama mahali pa kujificha na upepo, mahali pa kujisitiri na dhoruba, maji mahali pakavu, na kivuli cha kujikinga na jua
-