Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Huwafedhehesha Wenye Kiburi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 7 “Siku ya BWANA [“Yehova,” “NW”] wa majeshi” inakuja. Itakuwa wakati wa Mungu kudhihirisha hasira yake “juu ya mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu na kuinuka, na juu ya mialoni yote ya Bashani; na juu ya milima mirefu yote, na juu ya vilima vyote vilivyoinuka; na juu ya kila mnara mrefu, na juu ya kila ukuta ulio na boma; na juu ya merikebu zote za Tarshishi, na juu ya kila taswira ipendezayo.” (Isaya 2:12-16) Naam, kila shirika lililoundwa na mwanadamu kama ishara ya majivuno yake na kila mtu asiyemwogopa Mungu zitashughulikiwa katika siku ya hasira ya kisasi ya Yehova. Hivyo, “majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.”—Isaya 2:17.

      8. Siku ya hukumu iliyotabiriwa yajaje juu ya Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K.?

      8 Siku ya hukumu iliyotabiriwa yaja juu ya Wayahudi mwaka wa 607 K.W.K. Mfalme Nebukadreza wa Babiloni anapoharibu Yerusalemu. Wakazi waona jiji lao wanalolipenda likichomeka, majengo yake yenye fahari yakiwa yamebomolewa, ukuta wake wenye nguvu ukiwa umevunjwa-vunjwa. Hekalu la Yehova limebomolewa likawa vifusi. Hazina zao wala magari yao havifai chochote katika ‘siku ya Yehova wa majeshi.’ Namna gani sanamu zao? Ni kama tu Isaya anavyotabiri: “Sanamu zitatoweka kabisa.” (Isaya 2:18) Wayahudi—kutia ndani wakuu na watu wenye uwezo—wapelekwa uhamishoni huko Babiloni. Yerusalemu lapaswa kubaki ukiwa kwa miaka 70.

  • Yehova Huwafedhehesha Wenye Kiburi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • “Siku ya Yehova” Inayokaribia

      10. Mitume Paulo na Petro huelekeza kwenye “siku [gani] ya Yehova”?

      10 Maandiko huelekeza kwenye “siku ya Yehova” itakayokuwa muhimu zaidi kuliko siku ya hukumu juu ya Yerusalemu na Yuda za kale. Mtume Paulo, chini ya upulizio, aliishirikisha “siku ya Yehova” inayokuja na kuwapo kwa Mfalme Yesu Kristo aliyetawazwa. (2 Wathesalonike 2:1, 2) Petro alizungumza kuhusu siku hiyo kwa kuhusiana na kuanzishwa kwa ‘mbingu mpya na dunia mpya ambamo uadilifu utakaa.’ (2 Petro 3:10-13) Hiyo ndiyo siku ambayo Yehova atatekeleza hukumu yake juu ya mfumo wote mwovu wa mambo, pamoja na Jumuiya ya Wakristo.

      11. (a) Ni nani ‘watakaoistahimili’ “siku ya Yehova” inayokuja? (b) Twaweza kumfanyaje Yehova awe kimbilio letu?

      11 “Ole wake siku hii!,” asema nabii Yoeli, “kwa maana siku ya BWANA [“Yehova,” NW] inakaribia, nayo itakuja kama uangamivu utokao kwake aliye Mwenyezi.” Kwa kuzingatia ukaribu wa “siku” hiyo, je, kila mtu hapaswi kuhangaikia usalama wakati wa kipindi hicho chenye kutia hofu? “Ni nani awezaye kuistahimili?” auliza Yoeli. Ajibu hivi: “BWANA atakuwa kimbilio la watu wake.” (Yoeli 1:15; 2:11; 3:16) Je, Yehova Mungu atakuwa kimbilio kwa wale wenye roho ya kiburi na wanaotumaini mali, uwezo wa kijeshi, na miungu iliyotengenezwa na wanadamu? Haiwezekani! Mungu aliwaacha hata watu wake waliochaguliwa walipotenda hivyo. Basi ni muhimu kama nini kwa watumishi wote wa Mungu ‘waitafute haki na kuutafuta unyenyekevu,’ na kuchunguza kwa uzito mahali ilipo ibada ya Yehova maishani mwao!—Sefania 2:2, 3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki